Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sehemu ya 1—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Ijapokuwa Charles Taze Russell alipata kujulikana sana kwa sababu ya hotuba zake za Biblia zilizotangazwa sana, kupendezwa kwake hakukuwa tu katika wasikilizaji wengi lakini katika watu. Hivyo, muda mfupi baada ya kuanza kutangaza Watch Tower katika 1879, alianza safari ndefu ili kutembelea vikundi vidogo vya wasomaji wa gazeti hilo na kuzungumza Maandiko pamoja nao.

      C. T. Russell alihimiza wale walioamini ahadi zenye thamani za Neno la Mungu wazishiriki pamoja na wengine. Wale ambao mioyo yao ilichochewa sana na yale waliyojifunza walionyesha bidii halisi katika kufanya hilohilo. Ili kusaidia kazi, habari iliyochapwa ilitolewa. Mapema katika 1881, idadi fulani ya trakti zilitokea. Kisha habari kutoka hizo iliunganishwa na habari zaidi ili kufanyiza kijitabu Food for Thinking Christians chenye habari nyingi zaidi, na nakala 1,200,000 zilitayarishwa ili zigawanywe. Lakini kikundi kidogo cha Wanafunzi wa Biblia (labda 100 wakati ule) kingewezaje kugawanya nakala hizo zote?

      Kufikia Waenda-Kanisani

      Baadhi yazo zilipewa watu wa ukoo na marafiki. Idadi fulani ya magazeti ya habari yalikubali kupeleka nakala moja kwa kila mmoja wa waandikishaji wayo. (Mkazo wa pekee ulitiwa kwenye magazeti ya kila juma na ya kila mwezi ili kwamba Food for Thinking Christians kiweze kufikia watu wengi walioishi katika maeneo ya mashambani.) Lakini ugawanyaji mwingi ulifanywa katika Jumapili kadhaa mfululizo mbele ya makanisa katika Marekani na Uingereza. Hakukuwa na Wanafunzi wa Biblia wa kutosha kufanya kazi yote wao binafsi, hivyo waliwalipa wengine ili wasaidie.

      Ndugu Russell alituma washirika wawili, J. C. Sunderlin na J. J. Bender, Uingereza ili kusimamia kazi ya kugawanya nakala 300,000 huko. Ndugu Sunderlin alienda London, hali Ndugu Bender alisafiri kwenda kaskazini katika Scotland na kisha akafanya kazi akielekea kusini. Majiji makubwa ndiyo yaliyokaziwa fikira zaidi. Kwa njia ya matangazo ya magazeti ya habari, watu wenye uwezo walipatikana, na mikataba ilifanywa pamoja nao wapate wasaidizi wa kutosha kugawanya mafungu yao ya nakala. Wagawanyaji karibu 500 waliajiriwa kazi katika London pekee. Kazi ilifanywa haraka, katika Jumapili mbili mfululizo.

      Mwaka huohuo, mipango ilifanywa ili Wanafunzi wa Biblia ambao wangeweza kutumia nusu au zaidi ya wakati wao katika kazi ya Bwana tu, wawe makolpota, wakigawanya fasihi kwa ajili ya funzo la Biblia. Watangulizi hao wa wale wanaojulikana leo kuwa mapainia walifikia ugawanyaji wenye kutokeza kikweli wa habari njema.

      Wakati wa mwongo uliofuata, Ndugu Russell alitayarisha trakti mbalimbali ambazo zingeweza kutumiwa kwa urahisi kueneza baadhi ya zile kweli za Biblia zenye kutokeza walizokuwa wamejifunza. Pia aliandika mabuku kadhaa ya Millenial Dawn (baadaye yaliitwa Studies in the Scriptures). Kisha akaanza kusafiri kwenye nchi nyinginezo ili aeneze evanjeli kibinafsi.

      Russell Asafiri Ng’ambo

      Katika 1891 alizuru Kanada, ambako kupendezwa kwa kutosha kulikuwa kumechochewa tangu 1880 hivi kwamba kusanyiko lililohudhuriwa na 700 lingeweza kufanywa sasa katika Toronto. Pia alisafiri Ulaya katika 1891 ili kuona ni jambo gani lingeweza kufanywa ili kusogeza mbele kuenezwa kwa kweli huko. Safari hiyo ilimpeleka Ireland, Scotland, Uingereza, nyingi za nchi za bara la Ulaya, Urusi (lile eneo liitwalo sasa Moldova), na Mashariki ya Kati.

      Alifikia mkataa gani baada ya kuwasiliana na watu katika safari hiyo? “Sisi hatukuona kufunguka au utayari kwa ajili ya kweli katika Urusi . . . Hatukuona jambo lolote la kututia moyo tutumainie vuno lolote katika Italia au Uturuki au Austria au Ujerumani,” akaripoti. “Lakini Norway, Sweden, Denmark, Uswisi, na hasa Uingereza, Ireland, na Scotland, ni mashamba yaliyo tayari na yanangojea kuvunwa. Mashamba hayo yaonekana yakilia, Njooni huku mtusaidie!” Hiyo ilikuwa ile enzi ambayo Kanisa Katoliki lilikuwa lingali likikataza usomaji wa Biblia, wakati Waprotestanti wengi walikuwa wakiacha makanisa yao, na wengi, wakikatishwa tamaa na makanisa, walikuwa wakikataa Biblia kabisa.

      Ili kusaidia wale watu waliokuwa na njaa kiroho, baada ya safari ya Ndugu Russell katika 1891, jitihada zilizoongezwa zilifanywa kutafsiri fasihi katika lugha za Ulaya. Pia, mipango ilifanywa ili kuchapa na kuweka akiba ya fasihi katika London ili fasihi hizo ziweze kupatikana kwa urahisi kwa matumizi katika Uingereza. Shamba la Uingereza, lilithibitika kwelikweli kuwa tayari kuvunwa. Kufikia 1900, tayari kulikuwa makutaniko tisa na jumla ya Wanafunzi wa Biblia 138—miongoni mwao makolpota fulani wenye bidii. Wakati Ndugu Russell alipotembelea Uingereza tena katika 1903, watu elfu moja walikusanyika katika Glasgow ili kumsikia akihutubu juu ya “Matumaini na Matarajio ya Mileani,” 800 walihudhuria katika London, na wasikilizaji 500 kufikia 600 katika miji mingine.

      Hata hivyo, katika kuthibitisha maoni ya Ndugu Russell, baada ya ziara yake miaka 17 ilipita kabla ya kutaniko la kwanza la Wanafunzi wa Biblia kuundwa katika Italia, katika Pinerolo. Vipi Uturuki? Wakati wa miaka ya mwisho-mwisho ya 1880, Basil Stephanoff alikuwa amehubiri katika Makedonia, katika ile iliyoitwa wakati ule Uturuki ya Ulaya. Ijapokuwa wengine walionekana kuonyesha kupendezwa, wengine kutoka katika wale waliodai kuwa ndugu walitoa ripoti za uwongo, zilizomfanya atiwe gerezani. Haikuwa mpaka 1909 kwamba barua kutoka kwa Mgiriki katika Smirna (sasa Izmir), Uturuki, iliripoti kwamba kikundi huko kilikuwa kikijifunza kwa uthamini vichapo vya Watch Tower. Kwa habari ya Austria, Ndugu Russell mwenyewe alirudi katika 1911 ili kutoa hotuba katika Vienna, ikawa tu kwamba mkutano ulikatizwa na wafanyaghasia. Katika Ujerumani pia, itikio lenye uthamini lilikuja hatua kwa hatua. Lakini Waskandinevia walionyesha kujua zaidi uhitaji wao wa kiroho.

  • Sehemu ya 1—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Ramani/Picha katika ukurasa wa 405]

      C. T. Russell binafsi alitoa hotuba za Biblia katika majiji zaidi ya 300 (katika maeneo yanayoonyeshwa kwa alama) katika Amerika Kaskazini na Karibea—katika mengi yayo mara 10 au 15

      [Ramani]

      (See publication)

      [Ramani katika ukurasa wa 407]

      (See publication)

      Safari za Russell za kwenda kuhubiri Ulaya, kwa kawaida kupitia Uingereza

      1891

      1903

      1908

      1909

      1910 (mara mbili)

      1911 (mara mbili)

      1912 (mara mbili)

      1913

      1914

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki