Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sehemu ya 1—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Kabla ya ile safari ya miezi minne ya ulimwengu ya halmashauri ya IBSA haijakamilishwa, Ndugu Russell alikuwa amepangia R. R. Hollister kuwa mwakilishi wa Sosaiti katika nchi za Mashariki na kuhakikisha kwamba kazi inafanywa ya kueneza kwa vikundi vya watu ujumbe wa uandalizi wa upendo wa Mungu wa Ufalme wa Kimesiya.

  • Sehemu ya 1—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Picha katika ukurasa wa 420]

      C. T. Russell na washirika sita walifunga safari ya ulimwenguni pote katika 1911-1912 ili kuendeleza kazi ya kuhubiri habari njema

  • Sehemu ya 1—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Safari ya Ulimwengu ili Kuendeleza Kuhubiriwa kwa Habari Njema

      Jitihada nyingine kubwa ilifanywa katika 1911-1912 ili kusaidia watu wa nchi za Mashariki. International Bible Students Association lilituma halmashauri ya wanaume saba, ikiongozwa na C. T. Russell, ili wao binafsi wakadirie hali huko. Kokote walikoenda walisema juu ya kusudi la Mungu la kuletea wanadamu baraka kwa njia ya Ufalme wa Kimesiya. Nyakati nyingine wasikilizaji wao walikuwa wachache, lakini katika Filipino na India, kulikuwa maelfu. Wao hawakuunga mkono kampeni iliyopendwa na wengi wakati huo katika Jumuiya ya Wakristo ya kukusanya pesa kwa ajili ya wongofu wa ulimwengu. Waliona kwamba jitihada iliyo nyingi ya wamishonari wa Jumuiya ya Wakristo ilitumiwa katika kuendeleza elimu ya kilimwengu. Lakini Ndugu Russell alisadiki kwamba walichohitaji watu kilikuwa “ile Gospeli ya uandalizi wa upendo wa Mungu wa Ufalme ujao wa Mesiya.” Badala ya kutarajia kuongoa ulimwengu, Wanafunzi wa Biblia walielewa kutoka kwa Maandiko kwamba jambo lililopasa kufanywa wakati huo lilikuwa kutoa ushahidi na kwamba hilo lingetumikia kusudi la kukusanya “wachaguliwa wachache kutoka kwa mataifa yote, jamaa, kabila na lugha ili kushiriki katika jamii ya Bibi-arusi wa [Kristo]—ili kukaa pamoja Naye katika kiti Chake cha ufalme wakati wa miaka elfu, wakishirikiana kuinua jamii nzima ya kibinadamu.”a—Ufu. 5:9, 10; 14:1-5.

      Baada ya kutumia wakati katika Japani, China, na Filipino, na kwingineko, hao washiriki wa halmashauri hiyo waliongeza kilometa 6,400 zaidi za safari katika India. Watu fulani mmoja-mmoja waliokuwa wakiishi India walikuwa wamesoma fasihi za Sosaiti nao walikuwa wameandika barua kuonyesha uthamini wao kwa ajili yayo mapema sana kama 1887. Kazi ya kutoa ushahidi kwa bidii ilikuwa imefanywa pia miongoni mwa watu wenye kusema lugha ya Tamil tangu 1905 na kijana mmoja mwanamume ambaye, akiwa mwanafunzi katika Amerika, alikuwa amekutana na Ndugu Russell naye akajifunza kweli.

  • Sehemu ya 1—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Ndugu Russell alikuwa amesafiri kutoa hotuba katika mamia ya majiji katika Marekani na Kanada, alikuwa amesafiri mara kadhaa kwenda Ulaya, alikuwa ametoa hotuba katika Panama, Jamaika, na Kuba, pamoja na majiji makuu ya nchi za Mashariki. Makumi ya maelfu ya watu walikuwa wamesikia hotuba zake za Biblia zenye kusisimua na walikuwa wameona akijibu hadharani kutoka kwa Maandiko maswali yaliyozushwa na marafiki na maadui pia. Kupendezwa kwingi kulikuwa kumechochewa kwa njia hiyo, na maelfu ya magazeti katika Amerika, Ulaya, Afrika Kusini, na Australia yalikuwa yakichapisha kwa ukawaida mahubiri ya Ndugu Russell. Mamilioni ya vitabu, pamoja na mamia ya mamilioni ya trakti na fasihi nyinginezo katika lugha 35, vilikuwa vimegawanywa na Wanafunzi wa Biblia.

      Ingawa fungu lake lilikuwa lenye kutokeza, si Ndugu Russell pekee aliyekuwa akihubiri. Wengine vilevile, waliotawanyika kotekote duniani, walikuwa wakiunganisha sauti zao wakiwa mashahidi wa Yehova na Mwana wake, Yesu Kristo.

  • Sehemu ya 1—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Mamilioni ya vitabu na mamia ya mamilioni ya trakti yalikuwa yamegawanywa kabla ya mwisho wa Nyakati za Mataifa. Kwa kuongezea hayo, kufikia 1913 magazeti ya habari mengi kama 2,000 yalikuwa yakitangaza kwa ukawaida mahubiri yaliyotayarishwa na C. T. Russell, na katika mwaka 1914 wasikilizaji wanaojumlika kuwa zaidi ya 9,000,000 katika mabara matatu waliona ile “Photo-Drama of Creation.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki