Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Yehova Mmoja” Anaikusanya Familia Yake
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Julai 15
    • Zaidi ya hayo, Paulo anatuhimiza tujitahidi sana “kuushika umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani.” (Soma Waefeso 4:1-3.) Kufuata shauri hilo kunatia ndani kukubali kuongozwa na roho ya Mungu na kuiruhusu itokeze tunda lake ndani yetu. Tunda hilo la roho linawasaidia watu kusuluhisha matatizo kati yao, tofauti na matendo ya mwili, ambayo sikuzote yanawatenganisha watu.

  • “Yehova Mmoja” Anaikusanya Familia Yake
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Julai 15
    • 9. Tunawezaje kujichunguza wenyewe ili kuona ikiwa ‘tunajitahidi sana kuushika umoja wa roho’?

      9 Kwa hiyo, kila mmoja wetu anahitaji kujiuliza hivi: ‘Ninajitahidi kadiri gani “kuushika umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani”? Ninafanya nini ninapokosana na mwingine? Je, ninawaeleza marafiki wangu wengi kuhusu matatizo hayo nikitazamia waniunge mkono? Je, ninatarajia wazee waingilie kati kwa niaba yangu badala ya mimi mwenyewe kujitahidi sana kurudisha uhusiano wenye amani pamoja na mtu huyo? Je, ninawaepuka watu tuliokosana nao ili tusizungumzie matatizo yetu, labda kwa kuhakikisha kwamba ninajitenga nao kadiri iwezekanavyo?’ Je, matendo kama hayo yanaonyesha kwamba tunatenda kupatana na kusudi la Yehova la kukusanya pamoja tena vitu vyote katika Kristo?

      10, 11. (a) Kuna umuhimu gani wa kuwa na amani pamoja na ndugu zetu? (b) Tunaweza kufanya nini ili kusitawisha amani na hivyo kupata baraka za kiroho?

      10 Yesu alisema hivi: “Basi, ikiwa unaleta zawadi yako kwenye madhabahu na hapo ukumbuke kwamba ndugu yako ana jambo fulani juu yako, acha zawadi yako hapo mbele ya madhabahu, na uende zako; kwanza fanya amani yako pamoja na ndugu yako, na ndipo, ukiisha kurudi, itoe zawadi yako. Uwe tayari kusuluhisha mambo upesi.” (Mt. 5:23-25) Yakobo aliandika kwamba “mbegu ya tunda la uadilifu hupandwa chini ya hali zenye amani kwa wale wanaofanya amani.” (Yak. 3:17, 18) Kwa hiyo, hatuwezi kudumisha mwenendo wa uadilifu katika mazingira yasiyokuwa na amani.

      11 Kwa mfano, katika nchi fulani ambazo zimeharibiwa na vita, inakadiriwa kwamba zaidi ya asilimia 35 ya ardhi ingelimwa ikiwa raia hawangekuwa na wasiwasi kuhusu mabomu ya ardhini. Bomu la ardhini likilipuka, wakulima hawalimi tena, na inakuwa vigumu kwa watu kulima vijijini, na hivyo miji inakosa chakula. Vivyo hivyo, inakuwa vigumu kwetu kukua kiroho ikiwa tuna tabia ambazo zinaweza kuvuruga amani kati yetu na ndugu zetu. Lakini ikiwa tunawasamehe wengine kwa wepesi na kuwatendea mambo mema, tunasitawisha hali ambazo zinaleta baraka kwelikweli.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki