-
Kushikilia kwa Imara Jina la YesuUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Epuka Farakano!
13. Ni maneno gani ya karipio ambayo Yesu anafuata kuwatolea Wakristo katika Pargamamu, na ni kwa nini kundi hilo liliyahitaji?
13 Yesu anakaripia zaidi Wakristo katika Pargamamu, akisema: “Vivyo wewe, pia, unao hao wanaoshikilia kwa imara lile fundisho la lile farakano la Nikolausi hali kadhalika.” (Ufunuo 2:15, NW) Hapo kwanza, Yesu amesifu Waefeso kwa kuchukia kwao matendo ya farakano hili. Lakini Wakristo katika Pargamamu wanahitaji shauri juu ya kufuliza kutunza kundi likiwa bila farakano. Uthabiti zaidi unahitajiwa katika kutegemeza viwango vya Kikristo ili ule umoja ambao Yesu alisali kwenye Yohana 17:20-23 uhifadhiwe. Inahitajiwa kabisa “kutia moyo kwa fundisho ambalo ni lenye afya na kukaripia pia wale wanaopinganisha maneno.”—Tito 1:9, NW.
14. (a) Tangu siku za mapema, kundi la Kikristo limelazimika kushindana na akina nani, na mtume Paulo aliwaelezaje? (b) Ni maneno gani ya Yesu yanayopasa kutiiwa na yeyote ambaye huenda ikawa ameelekea kufuata kikundi chenye kujitenga mbali?
14 Tangu siku za mapema, kundi la Kikristo limekuwa halina budi kushindana na waasi-imani wenye kiburi, ambao kwa usemi laini, wenye kudanganya “husababisha migawanyiko na sababu za kukwaza kinyume cha fundisho” lililoandaliwa kupitia mfereji wa Yehova. (Waroma 16:17, 18, NW) Mtume Paulo alionya juu ya tisho hili karibu katika barua zake zote.a Katika nyakati za ki-siku-hizi, wakati ambapo Yesu amerudishia kundi la Kikristo la kweli usafi na umoja walo, hatari ya farakano inabaki. Kwa sababu hiyo, yeyote ambaye huenda alikuwa ameelekea kufuata kikundi chenye kujitenga mbali, hivyo kufanyiza farakano, apaswa atii maneno yafuatayo ya Yesu: “Kwa hiyo tubu. Usipofanya hivyo, mimi naja kwako upesi, nami nitapiga vita nao kwa upanga mrefu wa kinywa changu.”—Ufunuo 2:16, NW.
15. Farakano linaanzishwaje?
15 Farakano linaanzishwaje? Pengine mwalimu fulani wa kujifanya anapanda mashaka, akibishia ukweli fulani wa Biblia (Kama vile kuwa kwetu sisi katika siku za mwisho), na hivyo kikundi kilicho kisehemu kinavunjika na kutoka kumfuata yeye. (2 Timotheo 3:1; 2 Petro 3:3, 4) Au mtu fulani anachambua ile njia ambayo katika hiyo Yehova anafanyiza kazi yake naye anavuta ile roho ya kutofanya mengi sana kwa kudai kwamba kwenda nyumba kwa nyumba na ujumbe wa Ufalme si njia ya Kimaandiko wala haihitajiwi kabisa. Kushiriki utumishi kama huo kufuatia kielelezo cha Yesu na mitume wake kungewaendeleza hawa wakiwa wanyenyekevu; hata hivyo, wao wanaona ni afadhali wajitenge na kujistarehesha, pengine wakisoma Biblia tu pindi kwa pindi wakiwa kikundi cha faragha. (Mathayo 10:7, 11-13; Matendo 5:42; 20:20, 21) Watu kama hao wanabuni mawazo yao wenyewe juu ya Ukumbusho wa Kifo cha Yesu, ile amri ya Kimaandiko ya kuepukana na damu, kusherehekea sikukuu, na tumizi la tumbako. Zaidi ya hilo, wao wanashushia heshima jina la Yehova; upesi sana wanaanguka na kurudi ndani ya njia zenye kuendekeza za Babuloni Mkubwa. Hata vibaya zaidi, baadhi yao wanasukumwa na Shetani wageukie na ‘kupiga watumwa wenzao,’ ambao wakati mmoja walikuwa ndugu zao.—Mathayo 24:49; Matendo 15:29; Ufunuo 17:5, NW.
16. (a) Kwa nini wale wanaoyumba-yumba kwa sababu ya uvutano wa waasi-imani inawapasa watubu upesi? (b) Ni nini litakalopata wale wanaokataa kutubu?
16 Wowote ambao wanayumba-yumba kwa sababu ya uvutano wa waasi-imani wapaswa wawe wepesi kutii mwito wa Yesu wa kutubu! Propaganda ya waasi-imani lazima ikataliwe kuwa ni sumu! Msingi wayo ni husuda na chuki, tofauti na zile kweli zenye uadilifu, safi, na zenye kupendeka ambazo Yesu analisha kundi lake. (Luka 12:42; Wafilipi 1:15, 16; 4:8, 9) Kwa habari ya wale wanaokataa kutubu kweli kweli Bwana Yesu ‘hupiga vita nao kwa upanga mrefu wa kinywa chake.’ Yeye anapepeta watu wake ili kuhifadhi ule umoja ambao kwa ajili yao yeye alisali wakati wa jioni yake ya mwisho pamoja na wanafunzi wake duniani. (Yohana 17:20-23, 26) Kwa kuwa waasi-imani wanakataa lile shauri lenye upendo na msaada unaotolewa na zile nyota zilizo kwenye mkono wake wa kulia, Yesu anawahukumu na kuwaadhibu “kwa ukali ulio mkubwa zaidi sana,” akiwaweka kwenye “giza nje.” Wanatengwa na ushirika, wasitende tena kama chachu miongoni mwa watu wa Mungu.—Mathayo 24:48-51; 25:30; 1 Wakorintho 5:6, 9, 13; Ufunuo 1:16, NW.
-