-
Unaweza ‘Kuifanikisha Njia Yako’ Jinsi Gani?Mnara wa Mlinzi—2011 | Juni 15
-
-
Je, Nifuatie Elimu ya Juu?
Mkristo ana wajibu wa Kimaandiko wa kuitunza familia yake, na hilo linatia ndani kutimiza mahitaji yao ya kimwili. (1 Tim. 5:8) Hata hivyo, je, kweli tunahitaji digrii ya chuo kikuu au chuo cha mafunzo ili kufanya hivyo?
Ni vizuri mtu afikirie kufuatia elimu ya juu kutakuwa na matokeo gani juu ya uhusiano wake pamoja na Yehova. Acheni tuchunguze mfano wa Kimaandiko ambao utatusaidia kuelewa jambo hilo.
Baruku alikuwa mwandishi wa nabii Yeremia. Wakati fulani, badala ya kukazia fikira mapendeleo ambayo alikuwa nayo ya kumtumikia Yehova, Baruku alianza kujitafutia mambo makuu. Yehova aliona jambo hilo na akamwonya hivi kupitia Yeremia: “Wewe unaendelea kujitafutia makuu. Usiendelee kuyatafuta.”—Yer. 45:5.
Ni ‘mambo gani makuu’ ambayo Baruku alikuwa akiendelea kutafuta? Huenda alishawishiwa kujitafutia umashuhuri katika mfumo wa mambo wa Kiyahudi. Au huenda mambo hayo makuu yalikuwa utajiri wa kimwili. Kwa vyovyote vile, aliacha kukazia fikira mambo ya maana zaidi, mambo yenye thamani kiroho. (Flp. 1:10) Hata hivyo, bila shaka Baruku alisikiliza onyo ambalo Yehova alitoa kupitia Yeremia na hivyo akaiokoa nafsi yake kama nyara.—Yer. 43:6.
Tunaweza kujifunza nini kutokana na simulizi hilo? Shauri ambalo Baruku alipewa linaonyesha kwamba kulikuwa na tatizo. Alikuwa akijitafutia mwenyewe mambo makuu. Ikiwa una njia ya kujitegemeza mwenyewe, je, kweli unahitaji kutumia wakati, pesa, na nguvu kupata elimu ya juu ili tu kutimiza miradi ya kibinafsi au kwa sababu wazazi au watu wengine wa ukoo wanataka ufanye hivyo?
Mfikirie Grzegorz, anayefanya kazi ya kutayarisha programu za kompyuta. Alishawishiwa na wafanyakazi wenzake, akaamua kupata elimu ya ziada ya pekee inayochukua muda mrefu. Baada ya muda hakuwa na wakati wa kufuatia mambo ya kiroho. Anakumbuka hivi: “Sikuzote dhamiri ilinisumbua. Dhamiri yangu ilinisumbua kwa sababu singeweza kufikia miradi yangu ya kiroho ambayo nilikuwa nimejiwekea.”
-
-
Unaweza ‘Kuifanikisha Njia Yako’ Jinsi Gani?Mnara wa Mlinzi—2011 | Juni 15
-
-
Elimu ya juu: Yesu alionya kuhusu ‘kutafuta utukufu wako mwenyewe.’ (Yoh. 7:18) Unapofanya uamuzi wowote kuhusu kiwango cha elimu ya kilimwengu ambacho utapata, je, ‘umehakikisha mambo yaliyo ya maana zaidi’?—Flp. 1:9, 10.
Grzegorz, ambaye anafanya kazi ya kutayarisha programu za kompyuta, alifanya mabadiliko fulani katika maisha yake. Alisema hivi: “Nilichukua kwa uzito mashauri ya wazee, nikarahisisha maisha yangu. Nilitambua kwamba sikuhitaji kupata elimu zaidi ya kilimwengu. Ningetumia wakati na nguvu zangu zote kupata elimu hiyo.” Grzegorz alishiriki zaidi katika utendaji wa kutaniko. Baada ya muda, alihitimu katika shule ambayo sasa inaitwa Shule ya Biblia ya Ndugu Waseja. Ndiyo, ‘alinunua wakati’ ili kuongeza elimu yake ya kimungu.—Efe. 5:16.
-
-
Unaweza ‘Kuifanikisha Njia Yako’ Jinsi Gani?Mnara wa Mlinzi—2011 | Juni 15
-
-
ELIMU YA JUU
▪ Ikiwa una njia ya kupata riziki, je, kweli unahitaji kutumia wakati, pesa, na nguvu zako kupata elimu zaidi ya kilimwengu?
▪ Je, kweli ni lazima uwe na digrii ya chuo fulani cha mafunzo au chuo kikuu ili kupata riziki?
▪ Je, hilo litakuzuia kuhudhuria mikutano?
▪ Je, ‘umehakikisha mambo yaliyo ya maana zaidi’?
▪ Je, unahitaji kutia nguvu uhakika wako katika uwezo wa Yehova wa kutimiza mahitaji yako?
-