-
Kushikilia kwa Imara Jina la YesuUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
‘Mana Iliyofichwa na Kijiwe cha Mviringo Cheupe’
17. Ni thawabu gani inayongojea Wakristo wapakwa-mafuta ‘wanaoshinda,’ na ni nini ambacho Wakristo katika Pargamamu walihitaji kushinda?
17 Thawabu tukufu inawangojea wote ambao hutii shauri la Yesu, linalotolewa kwa mwelekezo wa roho takatifu ya Yehova. Sikiliza! “Acheni yeye ambaye ana sikio asikie ambacho roho husema kwa makundi: Yeye ambaye anashinda mimi nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa kijiwe cha mviringo cheupe, na juu ya kijiwe cha mviringo cheupe jina mpya lililoandikwa ambalo hakuna mmoja anayejua isipokuwa yeye anayelipokea.” (Ufunuo 2:17, NW) Hivyo, Wakristo katika Pargamamu kama vile wale Wakristo katika Smirna, wanatiwa moyo ‘washinde.’ Ikiwa watafanikiwa, wale walioko Pargamamu, ambako kuna kiti cha ufalme cha Shetani, lazima waepuke ibada ya sanamu. Lazima washinde ukosefu wa adili, farakano, na uasi-imani unaounganishwa na Balaki, Balaamu, na lile farakano la Nikolausi. Wakifanya hivyo, Wakristo hao wapakwa-mafuta wataalikwa wale baadhi ya “ile mana iliyofichwa.” Hii inamaanisha nini?
18, 19. (a) Ni nini iliyokuwa mana ambayo Yehova aliandalia Waisraeli? (b) Ni mana gani iliyofichwa? (c) Ni nini linalofananishwa na kula baadhi ya ile mana iliyofichwa?
18 Katika siku ya Musa, Yehova aliandaa mana kuendeleza Waisraeli wakati wa safari yao ya jangwani. Mana hiyo haikufichwa, kwa kuwa kila asubuhi—isipokuwa Sabato—ilitokea kimuujiza, kama sakitu yenye vipande vipande vyembamba vyenye kufunika ardhi. Lilikuwa andalio la kimungu ili kuendeleza hai Waisraeli. Ili iwe ukumbusho, Yehova alimwamuru Musa aweke baadhi ya huu “mkate” katika chupa ya dhahabu ndani ya lile sanduku takatifu la agano “katika vizazi vyote [vya Israeli].”—Kutoka 16:14, 15, 23, 26, 33; Waebrania 9:3, 4, NW.
19 Ni mfano wenye kufaa kama nini! Mana hii ilifichwa ndani ya chumba cha Patakatifu Zaidi Sana cha ile hema, ambamo ile nuru ya kimuujiza ambayo ilining’inia juu ya kifuniko cha lile sanduku ilifananisha kuwapo kwenyewe kwa Yehova. (Kutoka 26:34) Hakuna mmoja aliyeruhusiwa kupenya ndani ya mahali hapo patakatifu ili ale mana hiyo iliyofichwa. Hata hivyo, Yesu alisema kwamba wafuasi wake wapakwa-mafuta wanaoshinda wangekula “ile mana iliyofichwa.” Kama vile Kristo aliyewatangulia, wao wanapata kuingia, “[si] katika patakatifu palipofanyika kwa mikono, ndio mfano wa patakatifu halisi; bali . . . mbinguni hasa.” (Waebrania 9:12, 24) Wakati wa ufufuo wao, wanavaa kutofisidika na kutokufa—andalio zuri ajabu la Yehova, linalofananishwa na kupewa kwao ile “mana iliyofichwa” isiyoweza kuharibika. Lo! kundi hilo dogo la washindi ni lenye pendeleo kama nini!—1 Wakorintho 15:53-57.
20, 21. (a) Ni nini inayofananishwa na kuwapa Wakristo wapakwa-mafuta kijiwe cha mviringo cheupe? (b) Kwa kuwa kuna vijiwe vya mviringo vyeupe 144,000 tu, ni tumaini gani ulilo nalo ule umati mkubwa?
20 Hawa pia wanapokea “kijiwe cha mviringo cheupe.” Katika mahakama za Kiroma vijiwe vya mviringo vyeupe vilitumiwa katika kupitisha hukumu.b Kijiwe cha mviringo cheupe kilimaanisha ondoleo la hatia, hali kijiwe cha mviringo cheusi kilimaanisha hukumu ya laana, mara nyingi ni ya kifo. Kwa kuwapa Wakristo katika Pargamamu “kijiwe cha mviringo cheupe” Yesu angeonyesha kwamba yeye anawahukumu wao kuwa wasio na hatia, wenye kutakata, na walio safi. Lakini maneno ya Yesu huenda yakawa na maana zaidi. Katika nyakati za Kiroma, vijiwe vya mviringo vyeupe vilitumiwa pia kuwa tikiti za kupata ruhusa ya kuingia kwenye matukio ya maana. Kwa hiyo kijiwe cha mviringo cheupe huenda kikaonyesha kitu fulani cha pekee sana kwa Mkristo mpakwa-mafuta mwenye kushinda—kuruhusiwa kwake kuingia mahali penye heshima katika mbingu kwenye arusi ya Mwana-Kondoo. Ni vijiwe vya mviringo vyeupe kama hivyo 144,000 tu vinavyoandaliwa.—Ufunuo 14:1; 19:7-9.
-
-
Kushikilia kwa Imara Jina la YesuUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
22, 23. Ni nini maana ya lile jina lililoandikwa juu ya kijiwe cha mviringo cheupe wanalopewa Wakristo wapakwa-mafuta, na hilo lapasa liandae kitia-moyo gani?
22 Ni nini lile jina jipya lenye kuandikwa juu ya kile kijiwe cha mviringo cheupe? Jina ni njia ya kutambulisha mtu na kumtofautisha huyo na wengine. Hawa Wakristo wapakwa-mafuta wanapokea kile kijiwe cha mviringo cheupe baada ya wao kumaliza mwendo wao wa kidunia wakiwa washindi. Kwa wazi, basi, lile jina juu ya kijiwe cha mviringo cheupe linahusiana na pendeleo lao la kuwa wameunganishwa na Yesu mbinguni—cheo cha ukaribu zaidi sana cha utumishi wa kifalme kinachopasa kuthaminiwa kabisa kabisa na kufurahiwa na wale tu wanaorithi Ufalme wa kimbingu. Kwa sababu hiyo, ni jina au mtajo wa ofisi, “ambalo hakuna mmoja anayejua isipokuwa yeye anayelipokea.”—Linga Ufunuo 3:12.
23 Lo! ni kichocheo kama nini kwa jamii ya Yohana ‘isikie ambacho roho husema kwa makundi’ na kukitumia!
-