-
Kufisha Babuloni MkubwaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Hawa watapigana na Mwana-Kondoo, lakini, kwa sababu yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme, Mwana-Kondoo atashinda wao. Pia, wale wenye kuitwa na wachaguliwa na waaminifu pamoja na yeye watafanya hivyo.”—Ufunuo 17:12-14, NW.
-
-
Kufisha Babuloni MkubwaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Lakini ndugu za Yesu, wabakio wa mbegu ya mwanamke, wangali duniani na inaonekana wazi wanaumizika. (Ufunuo 12:17) Nyingi za pembe zimekwisha onyesha uhasama mkali kuwaelekea, na katika njia hii zimepigana na Mwana-Kondoo. (Mathayo 25:40, 45) Ingawa hivyo, karibuni, wakati utakuja wa Ufalme wa Mungu ‘kuponda-ponda na kuweka mwisho kwenye falme hizi zote.’ (Danieli 2:44, NW) Ndipo, wafalme wa dunia watakuwa katika pigano hadi tamati pamoja na Mwana-Kondoo, kama tutakavyoona karibuni. (Ufunuo 19:11-21) Lakini hapa tunajifunza mambo ya kutosha kung’amua kwamba mataifa hayatafanikiwa. Ingawa hayo pamoja na hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu wa UM wana “fikira moja” yao, wao hawawezi kumshinda “Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme” aliye mkubwa, wala hawawezi kushinda “wale wenye kuitwa na wachaguliwa na waaminifu pamoja na yeye,” kutia ndani wafuasi wapakwa-mafuta wake ambao wangali duniani. Hawa pia watakuwa wamekwisha shinda kwa kushika ukamilifu katika kujibu mashtaka maovu ya Shetani.—Warumi 8:37-39; Ufunuo 12:10, 11.
-