-
Je, Unaweza Kutegemea Mashauri ya Biblia?Amkeni!—2007 | Novemba
-
-
Shauri Linalobadili Maisha
“Nilikuwa mtu mwenye hasira sana,” anasema Gabriel, mwanamume kutoka India. “Nilipokasirishwa, ningepiga kelele, ningetupa-tupa vitu, na hata kuwaumiza watu. Funzo la Biblia lilinisaidia niweze kudhibiti hasira yangu. Sasa, hata hali iweje, ninaweza kujidhibiti.”
Gabriel alikuwa amesoma maandiko kama andiko la Methali 16:32, ambalo linasema hivi: “Asiye mwepesi wa hasira ni bora kuliko mwanamume mwenye nguvu, naye anayezuia roho yake ni bora kuliko mtu anayeteka jiji.” Mwanamume mwingine aitwaye Dhiraj, ambaye pia ameweza kuidhibiti hasira yake, anaeleza hivi, “Andiko hilohilo lilinisaidia kuona kwamba kuongozwa na hasira ni ishara ya udhaifu lakini kuidhibiti hasira ni ishara ya kujiweza.”
-
-
Je, Unaweza Kutegemea Mashauri ya Biblia?Amkeni!—2007 | Novemba
-
-
[Picha katika ukurasa wa 24]
Dhiraj, India
[Picha katika ukurasa wa 24]
Gabriel, India
-