-
“Hamwijui Ile Siku Wala Saa”Mnara wa Mlinzi—2012 | Septemba 15
-
-
1-3. (a) Ni hali gani zinazoonyesha somo la mifano miwili ambayo Yesu alitoa? (b) Tunahitaji kujibu maswali gani?
WAZIA kwamba ofisa fulani mashuhuri anakuomba umpeleke kwa gari kwenye mkutano muhimu. Hata hivyo, dakika chache kabla ya kwenda kumchukua ili umpeleke kwenye mkutano huo, unagundua kwamba gari halina mafuta ya kutosha. Unahitaji kwenda haraka kuongeza mafuta. Unapoenda, ofisa huyo anawasili. Anakutafuta kila mahali lakini hakupati. Hawezi kungoja, kwa hiyo, anamwomba dereva mwingine ampeleke kwenye mkutano huo. Punde si punde, unafika na kugundua kwamba ofisa huyo alienda zake na kukuacha. Ungehisije?
-
-
“Hamwijui Ile Siku Wala Saa”Mnara wa Mlinzi—2012 | Septemba 15
-
-
3 Katika mifano yake kuhusu mabikira na talanta, Yesu alitumia hali zinazofanana na hizo ili kuonyesha kwa nini katika nyakati za mwisho, baadhi ya Wakristo watiwa-mafuta wangethibitika kuwa waaminifu na wenye busara, lakini wengine hawangekuwa hivyo.a (Mt. 25:1-30) Alikazia somo la mifano hiyo kwa kusema hivi: “Kwa hiyo, endeleeni kukesha kwa sababu hamwijui ile siku wala saa,” yaani, wakati ambapo kwa kweli Yesu atakuja kutekeleza hukumu ya Mungu juu ya ulimwengu wa Shetani. (Mt. 25:13)
-