-
Je, Ni Mafundisho ya Uwongo Au ya Kweli?—Ukweli Kumhusu YesuMnara wa Mlinzi—2010 | Aprili 1
-
-
FUNDISHO: Yesu hakuwa na ndugu wala dada.
NI UWONGO.
Vitabu vya Injili vinaonyesha wazi kwamba Yesu alikuwa na ndugu na dada. Injili ya Luka inamwita Yesu “mzaliwa wa kwanza” wa Maria, kuonyesha kwamba alizaa watoto wengine baadaye.c (Luka 2:7) Injili ya Marko inataja kwamba watu fulani katika jiji la Nazareti walimwona Yesu kuwa mtu wa kawaida tu, aliyekuwa sawa na ndugu na dada zake. Waliuliza hivi: “Je, Yakobo, Yosefu, Yuda na Simoni si ndugu zake? Je, si dada zake wanaishi hapa katika mji wetu?”—Marko 6:3, Contemporary English Version; Mathayo 12:46; Yohana 7:5.
Tofauti na yale ambayo vitabu vya Injili vinasema, wanatheolojia wengi wanadai kwamba Yesu alikuwa mzaliwa wa pekee wa Maria. Baadhi yao wanasema kwamba ndugu na dada za Yesu wanaotajwa katika Biblia ni binamu zake.d Wengine hufikiri kwamba ndugu na dada hao wa Yesu ni watoto wa kambo wa Maria. Lakini fikiri hili: Ikiwa Yesu hakuwa na ndugu au dada, je, watu hao wa Nazareti wangesema maneno waliyosema? Kinyume chake, yaelekea baadhi yao walimwona Maria alipokuwa na mimba za watoto wale wengine. Walijionea kwa macho yao kwamba Yesu alikuwa mmoja kati ya watoto wengi ambao Maria alizaa.
-
-
Je, Ni Mafundisho ya Uwongo Au ya Kweli?—Ukweli Kumhusu YesuMnara wa Mlinzi—2010 | Aprili 1
-
-
d Wazo hili lililoungwa mkono na Jerome yapata mwaka wa 383 W.K. linapendwa na watu wengi wanaoamini kwamba Maria alibaki bikira maisha yake yote. Ingawa baadaye Jerome alitilia shaka wazo hili, watu wengi bado wanaliamini. Huo pia ndio msimamo wa Kanisa Katoliki.
-