-
Ufalme wa Mungu Wazaliwa!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Na mimi nikasikia sauti kubwa katika mbingu ikisema: ‘Sasa kumetukia wokovu na nguvu na ufalme wa Mungu wetu na mamlaka ya Kristo wake, kwa sababu mshtaki wa ndugu zetu amevurumishwa chini, ambaye huwashtaki mchana na usiku mbele za Mungu wetu!
-
-
Ufalme wa Mungu Wazaliwa!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
18 Ni ya nani sauti kubwa hiyo ambayo Yohana anasikia? Biblia haisemi. Lakini kilio kama hicho kinachoripotiwa kwenye Ufunuo 11:17 kilikuja kutoka kwa wazee 24 waliofufuliwa wakiwa katika vyeo vyao vya kimbingu, ambako sasa wao wanaweza kuwakilisha watakatifu 144,000. (Ufunuo 11:18) Na kwa kuwa watumishi wapakwa-mafuta wa Mungu wanaonyanyaswa ambao wangali duniani wanasemwa hapa kuwa “ndugu zetu,” taarifa hiyo ingeweza kwa uzuri kutoka kwa chimbuko lile lile. Hapana shaka kwamba hawa waaminifu wanaweza kuunga sauti zao, kwa kuwa ufufuo wao ungefuata upesi baada ya Shetani na magenge yake ya roho waovu kuwa wametupwa nje ya mbingu.
-