-
Ukristo Ukitenda Katikati ya MsukosukoMnara wa Mlinzi—1998 | Januari 15
-
-
Kukagua Uhitaji
Mashahidi wa Yehova katika Ulaya waliitikia tena huo uhitaji kwa uharaka. Kufikia Aprili 1997 kikoa cha kutoa msaada cha Mashahidi kilichotia ndani madaktari wawili wa kitiba kilikuwa kimekuja kwa ndege kikiwa na dawa na fedha. Katika Goma Mashahidi wenyeji tayari walikuwa wamepata halmashauri za kutoa msaada zikague hiyo hali ili msaada wa papo hapo uweze kutolewa. Hicho kikoa kililichunguza hilo jiji na maeneo yaliyolizunguka. Wajumbe walitumwa ili kupata ripoti kutoka sehemu za mbali zaidi. Habari ilipatikana pia kutoka Kisangani, umbali wa zaidi ya kilometa 1,000 magharibi mwa Goma. Ndugu wenyeji walisaidiwa kusimamia jitihada za kutoa msaada katika Goma, ambako Mashahidi 700 huishi.
Mmoja wa wazee Wakristo katika Goma alisema hivi: “Tulichochewa sana kuona ndugu zetu waliokuwa wamekuja kutoka mbali sana ili kutusaidia. Kabla hawajaja, tulisaidiana. Ndugu walilazimika kukimbia kutoka mashambani kwenda Goma. Baadhi yao walikuwa wamepoteza nyumba zao, na waliacha mashamba yao. Tuliwachukua nyumbani mwetu na kushiriki nao mavazi yetu na chakula kidogo tulichokuwa nacho. Yale ambayo tungeweza kufanya mahali hapa hayakuwa mengi. Baadhi yetu tulikuwa tukiugua kutokana na utapiamlo.
“Hata hivyo, ndugu kutoka Ulaya walileta fedha zilizotuwezesha kununua chakula, kilichokuwa adimu na ghali sana. Hicho chakula kilikuja wakati wa maana sana, kwa kuwa wengi hawakuwa na chakula chochote nyumbani mwao. Tuligawanya hicho chakula kwa Mashahidi na wasio Mashahidi. Ikiwa huo msaada haukuja wakati ambapo ulikuja, wengi zaidi wangalikufa, hasa watoto. Yehova aliwaokoa watu wake. Wasio Mashahidi walivutiwa sana. Wengi wao walieleza juu ya muungano na upendo wetu. Baadhi yao walikiri kwamba dini yetu ndiyo ya kweli.”
Ingawa chakula kilinunuliwa mahali hapo na dawa zilitumiwa, mengi zaidi yalihitajiwa. Kulikuwa na uhitaji wa mavazi na mablanketi, na vilevile ugavi mkubwa zaidi wa chakula na dawa. Usaidizi ulihitajiwa pia ili kujenga upya nyumba zilizokuwa zimeharibiwa.
-
-
Ukristo Ukitenda Katikati ya MsukosukoMnara wa Mlinzi—1998 | Januari 15
-
-
Ugawanyaji Katika Kongo
Bidhaa zilipoanza kufika Kongo, ndugu wawili na dada mmoja walikuja kutoka Ufaransa ili kufanya kazi na halmashauri za kutoa msaada za huko. Kuhusu shukrani zilizoonyeshwa na Mashahidi wa Kongo, Joseline alisema hivi: “Tulipokea barua nyingi za kuonyesha uthamini. Dada mmoja maskini alinipa kipambo cha malakiti. Wengine walitupatia picha zao wenyewe. Tulipokuwa tukiondoka, dada walinibusu, kunikumbatia, na kutoa machozi. Nilitoa machozi pia. Wengi walitoa maelezo kama vile, ‘Yehova ni mwema. Yehova hutufikiria.’ Kwa hiyo wao watambua kwamba Mungu astahili kusifiwa kwa ajili ya utoaji huo. Tulipokuwa tukigawanya chakula, ndugu na dada walimsifu Yehova kwa nyimbo za Ufalme. Lilikuwa jambo lenye kutia huruma sana.”
Daktari wa kitiba aitwaye Loic alikuwa mshiriki wa kikoa hicho. Wengi walimiminika ndani ya Jumba la Ufalme na kungojea kwa subira zamu yao ya kupata msaada wake. Akitaka kufanya jambo fulani pia, dada mmoja Mkongo alitayarisha na kuchanga maandazi 40 kwa ajili ya wale waliokuwa wakingojea kumwona daktari. Kwa kuwa watu wapatao 80 walikuwa wakingojea, kila mmoja wao alipokea andazi nusu.
Msaada kwa Wasio Mashahidi
Msaada huo wa huruma haukupewa Mashahidi wa Yehova pekee. Wengine pia walinufaika, kama vile wengi walivyonufaika mwaka wa 1994. Hilo lapatana na andiko la Wagalatia 6:10, ambalo lataarifu hivi: “Basi, kwa kweli maadamu tuna wakati wenye kufaa kwa ajili ya hilo, acheni sisi tufanye lililo jema kuelekea wote, lakini hasa kuelekea wale ambao katika imani ni jamaa zetu.”
Mashahidi waligawa dawa na mavazi kwenye shule kadhaa za msingi na makao ya watoto yatima karibu na Goma. Hayo makao ya watoto yatima ni nyumba ya watoto 85. Katika safari ya mapema zaidi ya kuchunguza hali, kikoa cha kutoa msaada kilizuru hayo makao ya watoto yatima na kuahidi kuwaletea ugavi wa masanduku 50 ya biskuti zenye kiwango cha juu cha protini, masanduku ya mavazi, mablanketi 100, dawa, na vichezeo. Hao watoto walipanga laini katika ua na kuwaimbia hao wageni. Kisha wakatoa ombi la pekee—je, wangeweza kuwa na mpira hivi kwamba wangeweza kucheza soka?
Majuma kadhaa baadaye hicho kikoa cha kutoa msaada kilitimiza ahadi zao za kuleta ugavi. Akiwa amevutiwa na ukarimu na yale aliyokuwa amesoma katika fasihi za Biblia alizokuwa amepewa, mkurugenzi wa hayo makao ya watoto yatima alisema kwamba alikuwa akielekea kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Na je, hao watoto walipewa mpira? “La,” akajibu Claude, msimamizi wa kikoa cha kutoa msaada kutoka Ufaransa. “Tuliwapa mipira miwili.”
Kambi za Wakimbizi
Msaada haukutolewa Kongo tu. Maelfu ya wakimbizi walikuwa wamekimbia kutoka katika kanda ya vita kwenda nchi jirani ambako kambi tatu za wakimbizi zilikuwa zimejengwa haraka-haraka. Mashahidi walisafiri kwenda huko, pia, ili kuona mambo ambayo yangeweza kufanywa. Ripoti hii ilipotayarishwa, hizo kambi zilikuwa kimbilio la wakimbizi 211,000, wengi wao kutoka Kongo. Wakimbizi wapatao 800 walikuwa Mashahidi na watoto wao na watu mmoja-mmoja wenye kupendezwa na habari njema ya Ufalme. Tatizo la papo hapo katika hizo kambi lilikuwa ukosefu wa chakula. Kwenye kambi moja, kulikuwa na chakula cha kutosha siku tatu tu, nacho kilitia ndani maharagwe yaliyokuwa yamekaa kwa miaka mitatu.
Hata hivyo, hao Mashahidi walikuwa na furaha. Ingawa walikuwa na fasihi chache za Biblia, waliongoza mikutano iliyofanyika nje kwa ukawaida ili kujijenga kiroho. Pia walikuwa wenye shughuli wakihubiria wengine kambini habari njema ya Ufalme wa Mungu.—Mathayo 24:14; Waebrania 10:24, 25.
Kikoa cha uchunguzi cha Mashahidi kilitia ndani daktari mmoja wa kitiba. Ingawa wenye mamlaka walikiruhusu kikoa hicho kitumie siku chache tu kwenye kila kambi, waliwasiliana kitiba. Waliwaachia wazee Wakristo dawa na fedha. Hivyo, ndugu waliweza kubaki hai. Pia walitumaini kwamba Mashahidi katika kambi mbalimbali wangeweza kurudi upesi katika nchi yao ya nyumbani.
-