Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kujenga Pamoja Duniani Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Wenye Kujitolea wa Kimataifa

      Kadiri uhitaji wa upanuzi wa kasi ulivyokua, mpango wa wenye kujitolea wa kimataifa ulianzishwa katika 1985. Hiyo kwa vyovyote haikuwa ndiyo mara ya kwanza kuwa na ushirikiano wa kimataifa katika ujenzi, lakini sasa mpango huo uliratibiwa kwa uangalifu kutoka makao makuu. Wote ambao hushiriki ni Mashahidi ambao hujitolea kusaidia kazi ya ujenzi nje ya nchi zao wenyewe. Wao ni wafanyakazi stadi, pamoja na wenzi wa ndoa ambao huenda pamoja na waume zao kusaidia kwa njia yoyote wawezayo. Walio wengi wao hulipia nauli zao wenyewe; hakuna wanaopewa mshahara kwa ajili ya kile wafanyacho. Baadhi yao huenda kwa muda mfupi, kwa kawaida wakikaa kuanzia majuma mawili hadi miezi mitatu. Wengine ni wenye kujitolea wa muda mrefu, wakikaa kwa mwaka au zaidi, labda mpaka ujenzi unapokamilika. Mashahidi wa Yehova zaidi ya 3,000 kutoka nchi mbalimbali 30 walishiriki sehemu katika kazi hiyo wakati wa miaka mitano ya kwanza, na wengi zaidi walikuwa na hamu ya kushiriki kadiri stadi zao zilivyohitajiwa. Wao hulihesabu kuwa pendeleo kujitoa wenyewe na mali zao ili kusogeza mbele masilahi ya Ufalme wa Mungu kwa njia hiyo.

      Wafanyakazi wa kujitolea wa kimataifa huandaliwa makao na milo. Mara nyingi starehe ni ndogo kabisa. Mashahidi wenyeji huthamini sana yale yanayofanywa na ndugu zao wenye kuzuru, na inapowezekana, wao huwakaribisha nyumbani mwao, hata iwe sahili namna gani. Mara nyingi sana milo huliwa kwenye mahali pa kazi.

      Ndugu wa kutoka ng’ambo hawawi hapo ili kufanya kazi yote. Lengo lao ni kufanya kazi pamoja na kikundi cha ujenzi cha wenyeji. Na mamia, hata maelfu, ya wengine katika nchi huenda pia wakaja kusaidia wakati wa miisho-juma au kwa juma moja au zaidi kwa wakati mmoja. Katika Argentina, wenye kujitolea 259 kutoka nchi nyingine walifanya kazi pamoja na maelfu kadhaa ya ndugu wenyeji, baadhi yao walikuwapo kwa ajili ya kazi kila siku, wengine kwa majuma machache, na wengine zaidi wakati wa miisho-juma. Katika Kolombia, wenye kujitolea wa kimataifa zaidi ya 830 walisaidia kwa vipindi mbalimbali vya wakati. Kulikuwa pia wenye kujitolea wenyeji zaidi ya 200 walioshiriki katika mradi huo kwa wakati wote, na wasaidizi wengine 250 au zaidi kila mwisho-juma. Jumla ya zaidi ya watu mmoja-mmoja tofauti 3,600 walishiriki.

      Tofauti ya lugha yaweza kutokeza matatizo, lakini haizuii vikundi vya kimataifa visifanye kazi pamoja. Lugha ya ishara, ishara za uso, ucheshi, na tamaa ya kuona kazi itakayomheshimu Yehova ikikamilishwa husaidia kazi ifanywe.

      Ukuzi wa tengenezo wenye kutokeza—ukitokeza uhitaji wa makao makubwa ya tawi—nyakati nyingine hutokea katika nchi ambako idadi ya watu wenye stadi katika ufundi wa ujenzi ni ndogo. Lakini hicho si kizuizi miongoni mwa Mashahidi wa Yehova, ambao husaidiana kwa furaha. Wao hufanya kazi pamoja wakiwa sehemu ya familia ya duniani pote ambayo haigawanywi na taifa, rangi ya ngozi, au lugha.

      Katika Papua New Guinea, wenye kujitolea waliotoka Australia na New Zealand kila mmoja alizoeza raia wa Papua New Guinea kazi yake ya kiufundi, kupatana na ombi la Idara ya Wafanyakazi ya Serikali. Katika njia hiyo, huku wakijitoa wenyewe, Mashahidi wenyeji walijifunza kazi za ufundi ambazo zingeweza kuwasaidia kutosheleza mahitaji yao wenyewe na ya familia zao.

      Wakati tawi jipya lilipohitajiwa katika El Salvador, wenye kujitolea 326 kutoka ng’ambo walijiunga na ndugu wenyeji. Kwa ajili ya mradi wa ujenzi katika Ekuado, Mashahidi 270 kutoka nchi 14 walifanya kazi pamoja na ndugu na dada Waekuado. Baadhi ya wenye kujitolea wa kimataifa walisaidia katika miradi kadhaa ya ujenzi iliyokuwa ikiendelea wakati uleule mmoja. Walifanya kazi kwa zamu katika mahali pa ujenzi katika Ulaya na Afrika, kulingana na uhitaji wa stadi zao za kiufundi.

      Kufikia 1992, wenye kujitolea wa kimataifa walikuwa wamepelekwa sehemu 49 za matawi ili kusaidia vikundi vya ujenzi vya wenyeji. Katika visa fulani wale waliopokea msaada kutokana na programu hii waliweza pia kuandaa usaidizi kwa wengine. Hivyo, wakiwa wamenufaika na kazi za bidii za watumishi wa muda mrefu wa kimataifa kama 60 waliosaidia na ujenzi wa mradi wa tawi katika Filipino, pamoja na wenye kujitolea zaidi ya 230 kutoka ng’ambo waliosaidia kwa vipindi vifupi zaidi, baadhi ya Wafilipino walijitoa wenyewe ili kusaidia kujenga vifaa katika sehemu nyingine za Kusini-Mashariki mwa Asia.

  • Kujenga Pamoja Duniani Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Picha katika ukurasa wa 338]

      Programu ya Ujenzi wa Kimataifa Hutimiza Mahitaji ya Haraka

      Ukuzi wa kasi wa tengenezo umetaka upanuzi wenye kuendelea wa ofisi, viwanda, na makao ya Betheli duniani pote

      Wenye kujitolea wa kimataifa hutoa usaidizi kwa Mashahidi wenyeji

      Hispania

      Njia za ujenzi zitumiwazo hufanya wenye kujitolea wengi wasiokuwa na ujuzi waweze kufanya kazi yenye thamani

      Puerto Riko

      Wafanyakazi stadi hutoa huduma zao kwa furaha

      New Zealand

      Ugiriki

      Brazili

      Matumizi ya vifaa vyenye kudumu husaidia kupunguza gharama za muda mrefu za udumishaji

      Uingereza

      Kazi bora sana hutokana na kupendezwa kwa binafsi kwa upande wa wenye kuifanya; hiyo ni wonyesho wa upendo wao kwa Yehova

      Kanada

      Ujenzi huo mbalimbali ni pindi za shangwe; urafiki mwingi wenye kudumu hufanyizwa

      Kolombia

      Ishara katika Japani zilikumbusha wafanyakazi juu ya hatua za usalama, pia juu ya uhitaji wa kuonyesha matunda ya roho ya Mungu

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki