-
“Wakati wa Amani” Umekaribia!Mnara wa Mlinzi—1999 | Oktoba 1
-
-
5. Wakristo wa kweli hawawezi kufanya nini kamwe?
5 Wakristo wa kweli hawawezi kamwe kupigana na wanadamu wenzao—kama vile ambavyo wale waitwao eti Wakristo wamefanya mara nyingi, hasa katika karne ya 20. (Yakobo 4:1-4) Ni kweli kwamba wao hupiga vita dhidi ya mafundisho yanayopotosha juu ya Mungu, lakini hiyo ni vita inayokusudiwa kuwasaidia watu, si kuwadhuru. Ni kinyume kabisa na Ukristo wa kweli kuwanyanyasa wengine kwa sababu ya tofauti za kidini au kuwadhuru watu kwa sababu za kizalendo. “Ikiwezekana, kwa kadiri itegemeavyo nyinyi,” Paulo akawaagiza Wakristo Waroma, “iweni wenye kufanya amani na watu wote.”—Waroma 12:17–19; 2 Timotheo 2:24, 25.
-
-
“Wakati wa Amani” Umekaribia!Mnara wa Mlinzi—1999 | Oktoba 1
-
-
Kwa Nini Uwe “Wakati wa Vita”?
7, 8. (a) Licha ya msimamo wao wa amani, Mashahidi wa Yehova huuonaje wakati wa sasa? (b) Ni nini iliyo silaha kuu katika shughuli ya vita ya Mkristo?
7 Licha ya msimamo wao wa amani, Mashahidi wa Yehova hata hivyo huuona wakati wa sasa kuwa hasa “wakati wa vita.” Bila shaka hii si shughuli ya vita halisi, kwa kuwa, kuwalazimisha wengine wakubali ujumbe wa Biblia kwa kutumia nguvu kungekuwa kinyume cha mwaliko wa Mungu wa “[ku]acha yeyote atakaye achukue maji ya uhai bure.” (Ufunuo 22:17) Watu hawalazimishwi kugeuza imani! Shughuli ya vita ya Mashahidi wa Yehova hasa ni ya kiroho. Paulo aliandika: “Silaha za shughuli yetu ya vita si za kimwili, bali zenye nguvu kupitia Mungu kwa ajili ya kupindua mambo yaliyotiwa kwa nguvu sana katika mahandaki.”—2 Wakorintho 10:4; 1 Timotheo 1:18.
8 “Upanga wa roho, yaani, neno la Mungu,” ndio silaha kuu kati ya “silaha za shughuli yetu ya vita.” (Waefeso 6:17) Upanga huo una nguvu. “Neno la Mungu liko hai na hukazia nguvu na ni lenye makali zaidi kuliko upanga wowote wenye makali kuwili na hudunga hata kufikia kugawanya nafsi na roho, na viungo na uloto wavyo, na ni lenye kuweza kufahamu fikira na makusudio ya moyo.” (Waebrania 4:12) Kwa kutumia upanga huo, Wakristo wanaweza kupindua “mawazowazo na kila jambo lililoinuka sana lililoinuliwa dhidi ya ujuzi wa Mungu.” (2 Wakorintho 10:5) Huo huwawezesha kufichua mafundisho yasiyo ya kweli, mazoea yenye kudhuru, na falsafa zinazoonyesha hekima ya mwanadamu badala ya hekima ya Mungu.—1 Wakorintho 2:6-8; Waefeso 6:11-13.
9. Kwa nini hatuwezi kulegea katika vita yetu dhidi ya mwili wenye dhambi?
9 Aina nyingine ya shughuli ya vita ya kiroho ni ile inayopigwa dhidi ya mwili wenye dhambi. Wakristo hufuata kielelezo cha Paulo, aliyekiri: “Napiga-piga mwili wangu ngumi na kuuongoza kama mtumwa, ili, baada ya mimi kuwa nimewahubiria wengine, mimi mwenyewe nisiwe mwenye kukataliwa kwa njia fulani.” (1 Wakorintho 9:27) Wakristo katika Kolosai walishauriwa kufisha “viungo vya mwili [wao] vilivyo juu ya dunia kwa habari ya uasherati, ukosefu wa usafi, hamu ya ngono, tamaa yenye kuumiza, na tamaa, ambako ni ibada ya sanamu.” (Wakolosai 3:5) Naye mwandishi wa Biblia, Yuda, akawahimiza Wakristo kwa bidii “[wa]fanye pigano kali kwa ajili ya imani ambayo ilikabidhiwa mara moja kwa wakati wote kwa watakatifu.” (Yuda 3) Kwa nini tufanye hivyo? Paulo ajibu: “Ikiwa mwaishi kupatana na mwili hakika nyinyi mtakufa; bali mkiua mazoea ya mwili kwa roho, mtaishi.” (Waroma 8:13) Kwa kuzingatia taarifa hiyo iliyo wazi, hatuwezi kulegea katika vita yetu dhidi ya mielekeo mibaya.
-