-
Alikaa Macho, na AlingojaMnara wa Mlinzi—2008 | Aprili 1
-
-
Alikaa Macho Akiwa na Uhakika
Eliya alikuwa na uhakika wa kwamba Yehova angekomesha ukame, lakini hakujua Yehova angefanya hivyo wakati gani. Nabii huyo alifanya nini alipokuwa akingoja? Ona jinsi mstari wa 43 unavyosema: “Akamwambia mtumishi wake: ‘Nenda juu, tafadhali. Tazama upande wa bahari.’ Basi akaenda juu, akatazama na kisha akasema: ‘Hakuna kitu chochote.’ Naye akaendelea kusema, ‘Rudi,’ mara saba.” Mfano wa Eliya unatufundisha angalau mambo mawili. Kwanza, ona uhakika wa nabii huyo. Kisha, fikiria jinsi alivyokaa macho.
-
-
Alikaa Macho, na AlingojaMnara wa Mlinzi—2008 | Aprili 1
-
-
Kisha, ona jinsi Eliya alivyokaa macho. Alimtuma mtumishi wake, si mara moja au mbili tu, bali mara saba! Tunaweza kuwazia kwamba mtumishi huyo alichoka kwa sababu ya kutumwa tena na tena, lakini Eliya alikuwa na hamu ya kuona ishara naye hakukata tamaa. Mwishowe, baada ya safari ya saba, mtumishi wake aliripoti hivi: “Tazama! Pana wingu dogo kama kiganja cha mkono wa mwanadamu linalopanda kutoka baharini.” (Mstari wa 44) Je, unaweza kumwona mtumishi huyo, akiunyoosha mkono wake na kuonyesha kwa kiganja chake ukubwa wa wingu dogo ambalo lilikuwa likipanda kutoka katika ile Bahari Kuu?b Huenda mtumishi huyo alifikiri wingu hilo halikuwa muhimu. Hata hivyo, Eliya aliona wingu hilo kuwa muhimu. Hivyo, akamwagiza haraka mtumishi wake: “Nenda juu, mwambie Ahabu, ‘Funga gari! Nawe ushuke ili mvua kubwa isikuzuie!’”
Katika kisa hiki pia, Eliya anatuwekea mfano mzuri sana. Sisi pia tunaishi wakati ambapo Mungu anakaribia kuchukua hatua ili kutimiza kusudi lake alilofunua. Eliya alingoja mwisho wa ukame; watumishi wa Mungu leo wanangoja mwisho wa ulimwengu huu wenye ufisadi. (1 Yohana 2:17) Tunapaswa kuendelea kukaa macho kama Eliya mpaka Yehova Mungu atakapochukua hatua. Yesu, Mwana wa Mungu, aliwashauri hivi wafuasi wake: “Kwa hiyo, endeleeni kukesha kwa sababu hamjui ni siku gani Bwana yenu atakuja.” (Mathayo 24:42) Je, Yesu alimaanisha kwamba wafuasi wake hawangejua kamwe wakati ambapo mwisho ungekuja? Hapana, kwa kuwa alizungumzia kwa urefu jinsi ambavyo hali ya ulimwengu ingekuwa kabla ya mwisho. Kila mmoja wetu anaweza kujifunza kuhusu ishara hiyo yenye mambo mengi ya “umalizio wa mfumo wa mambo.”—Mathayo 24:3-7.c
-