Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutumikia Pamoja na Mlinzi
    Mnara wa Mlinzi—2000 | Januari 1
    • Miaka ipatayo 200 kabla ya tukio hilo, Yehova aliamuru hivi: “Enenda, weka mlinzi; aonayo na ayatangaze.” Mlinzi huyo alikuwa na habari gani za kutangaza? “Babeli umeanguka, umeanguka; na sanamu zote za miungu yake zimevunjwa chini.” (Isaya 21:6, 9) Kwa hiyo, mwaka wa 539 K.W.K., tangazo hilo la unabii likatimia. Babiloni lenye nguvu lilianguka, na punde si punde watu wa agano wa Mungu wakarudi nchini kwao.

  • Kutumikia Pamoja na Mlinzi
    Mnara wa Mlinzi—2000 | Januari 1
    • “Mlinzi” Akaa Macho

      12. Ni nani leo walio jamii ya mlinzi, nao wamekuwa na mtazamo gani?

      12 Basi, “wakati wa mwisho” ulipoanza, mara nyingine tena Yehova akamtokeza mlinzi, anayewatolea watu onyo juu ya matukio yahusuyo utimizo wa makusudi Yake. (Danieli 12:4; 2 Timotheo 3:1) Hadi leo hii, jamii hiyo ya mlinzi—Wakristo watiwa-mafuta, Israeli wa Mungu—imekuwa ikitenda kupatana na ufafanuzi wa unabii wa Isaya kuhusu mlinzi: “[Alisikiliza] sana, akijitahidi kusikiliza. Ndipo akalia kama simba, Ee Bwana, mimi nasimama daima juu ya mnara wakati wa mchana, na kila usiku ninakaa katika zamu ya ulinzi wangu.” (Isaya 21:7, 8) Huyo ni mlinzi anayechukua kazi yake kwa uzito!

      13. (a) Mlinzi wa Yehova ametangaza ujumbe gani? (b) Inaweza kusemwaje kwamba Babiloni Mkubwa ameanguka?

      13 Mlinzi huyo aliona nini? Mara nyingine tena, mlinzi wa Yehova, jamii yake ya shahidi, alitangaza hivi: “Babeli umeanguka, umeanguka; na sanamu zote za miungu yake [Yehova amezivunja] chini”! (Isaya 21:9) Mara hii, baada ya Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, ni Babiloni Mkubwa, milki ya ulimwengu ya dini isiyo ya kweli, anayenyang’anywa mamlaka yake. (Yeremia 50:1-3; Ufunuo 14:8) Si ajabu! Vita Kubwa, kama ilivyojulikana wakati huo, ilianzia katika Jumuiya ya Wakristo, ambako makasisi wa pande zote walichochea mapigano kwa kuwatia moyo vijana wao wenye nguvu waende vitani. Ni aibu iliyoje! Mwaka wa 1919, Babiloni Mkubwa hangeweza kuwazuia Wanafunzi wa Biblia, kama vile Mashahidi wa Yehova walivyojulikana wakati huo, wasitoke katika hali yao ya kutotenda na kuanza kampeni ya kutoa ushahidi ulimwenguni kote ambayo bado yaendelea. (Mathayo 24:14) Jambo hilo likawa ishara ya kuanguka kwa Babiloni Mkubwa, kama vile tu kuachiliwa kwa Israeli katika karne ya sita K.W.K. kulivyokuwa ishara ya kuanguka kwa Babiloni la kale.

      14. Jamii ya mlinzi ya Yehova imetumia gazeti gani kwa njia yenye kutokeza, na Yehova amebarikije utumizi wake?

      14 Nyakati zote jamii ya mlinzi imefanya kazi yake kwa bidii ikiwa na hamu kubwa ya kufanya lililo jema. Mwezi wa Julai 1879, Wanafunzi wa Biblia walianza kuchapisha gazeti hili, ambalo wakati huo liliitwa Zion’s Watch Tower and Herald of Christ’s Presence. Kila toleo tangu mwaka wa 1879 hadi Desemba 15, 1938, lilikuwa na maneno haya kwenye jalada la mbele “‘Ee Mlinzi, Habari Gani za Usiku?’—Isaya 21:11.”a Kwa miaka 120, gazeti la Mnara wa Mlinzi limekuwa likilinda kwa uaminifu juu ya matukio ya ulimwengu na maana yake ya unabii. (2 Timotheo 3:1-5, 13) Jamii ya Mungu ya mlinzi na waandamani wake wa “kondoo wengine” wametumia gazeti hili kutangazia wanadamu kwa bidii kwamba utetezi wa enzi kuu ya Yehova kupitia Ufalme wa Kristo u karibu. (Yohana 10:16) Je, Yehova amelibariki gazeti hili? Naam, tangu toleo la kwanza la nakala 6,000 mwaka wa 1879, gazeti la Mnara wa Mlinzi limeongezeka kufikia nakala zaidi ya 22,000,000 zinazopelekwa ulimwenguni kote katika lugha 132—na lugha 121 kati ya hizo huchapishwa sawia. Basi yafaa kama nini kwamba gazeti la kidini lenye kuenezwa kwa wingi zaidi ya yote duniani liwe gazeti ambalo latukuza jina la Mungu wa kweli, Yehova!

      Utakasaji Wenye Kuendelea

      15. Ni utakasaji gani wenye kuendelea ulioanza hata kabla ya mwaka wa 1914?

      15 Kwa miaka ipatayo 40 hadi utawala wa mbinguni wa Kristo ulipoanza mwaka wa 1914, Wanafunzi wa Biblia walikuwa wamewekwa huru kutoka kwa mafundisho mengi yasiyo ya Kibiblia ya Jumuiya ya Wakristo, kama vile ubatizo wa vitoto vichanga, kutokufa kwa nafsi ya mwanadamu, purgatori, moto wa helo, na Mungu wa Utatu. Lakini ilichukua muda zaidi kuondoa mawazo yote yenye makosa. Kwa kielelezo, katika miaka ya 1920 Wanafunzi wengi wa Biblia walivaa nembo yenye msalaba na taji, nao walisherehekea Krismasi na sikukuu nyingine za kipagani. Hata hivyo, ili ibada iwe safi, ni sharti vitu vyote vya ibada ya sanamu vitupiliwe mbali. Sharti Neno la Mungu, Biblia Takatifu, liwe msingi pekee wa imani ya Mkristo na njia yake ya maisha. (Isaya 8:19, 20; Waroma 15:4) Ni makosa kuongeza au kuondoa chochote kutoka kwenye Neno la Mungu.—Kumbukumbu la Torati 4:2; Ufunuo 22:18, 19.

      16, 17. (a) Jamii ya mlinzi ilishikilia dhana gani isiyo ya kweli kwa miongo kadhaa? (b) Ni maelezo gani yaliyo sahihi kuhusu “madhabahu” na “nguzo” katika “Misri”?

      16 Kielelezo kimoja kitakazia umuhimu wa kanuni hiyo. Mwaka wa 1886 C. T. Russell alipochapisha kitabu ambacho kilikuja kuitwa The Divine Plan of the Ages, buku hilo lilikuwa na ramani iliyohusianisha vizazi vya mwanadamu na Piramidi Kuu ya Misri. Ilidhaniwa kwamba piramidi hiyo ya kumkumbuka Farao Khufu ndiyo nguzo inayotajwa kwenye Isaya 19:19, 20: “Katika siku hiyo itakuwako madhabahu katika nchi ya Misri kwa BWANA, na nguzo mpakani mwake kwa BWANA. Nayo itakuwa ishara na ushuhuda kwa BWANA wa majeshi katika nchi ya Misri.” Piramidi hiyo ingekuwa na uhusiano gani na Biblia? Basi, kwa kielelezo, ilidhaniwa kuwa urefu wa vijia fulani katika Piramidi Kuu hiyo ulidokeza wakati wa mwanzo wa “dhiki kubwa” ya Mathayo 24:21, kama ilivyoeleweka wakati huo. Baadhi ya Wanafunzi wa Biblia wakaanza kujishughulisha sana kupima sehemu mbalimbali za piramidi hiyo ili kubainisha mambo kama vile siku watakapoenda mbinguni!

      17 Hiyo Piramidi Kuu iliheshimiwa sana kwa miongo kadhaa, hadi matoleo ya Mnara wa Mlinzi ya Novemba 15 na Desemba 1, 1928, yaliposema waziwazi kwamba Yehova hahitaji nguzo ya jiwe iliyojengwa na mafarao wapagani na yenye ishara za roho waovu za unajimu ili kuthibitisha ushahidi ulio katika Biblia. Badala yake, ilitambuliwa kwamba unabii wa Isaya una utimizo wa kiroho. Kama ilivyo katika Ufunuo 11:8, “Misri” ni mfano wa ulimwengu wa Shetani. ‘Madhabahu hiyo kwa BWANA’ yatukumbusha dhabihu zenye kukubalika zinazotolewa na Wakristo watiwa-mafuta wakiwa wangali wakazi wa muda katika ulimwengu huu. (Waroma 12:1; Waebrania 13:15, 16) Nguzo iliyo ‘mpakani mwa Misri’ hurejezea kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta, ambalo ni “nguzo na tegemezo la ile kweli” nalo ni ushahidi katika “Misri,” ulimwengu ambao watauacha hivi karibuni.—1 Timotheo 3:15.

      18. (a) Yehova ameendeleaje kufanya mambo yawe wazi zaidi kwa wanafunzi wa Biblia wenye mioyo minyofu? (b) Ikiwa Mkristo aona kuwa maelezo fulani mapya ya Maandiko ni magumu kuelewa, apaswa kuwa na mtazamo gani wenye hekima?

      18 Miaka isongapo, Yehova aendelea kufanya kweli iwe wazi, kutia ndani kufanya neno lake la unabii kuwa wazi zaidi. (Mithali 4:18) Katika miaka ya hivi majuzi, tumetiwa moyo kuangalia tena kwa uelewevu zaidi—miongoni mwa mambo mengine—kizazi ambacho hakitapitilia mbali kabla ya mwisho kuja, mfano wa kondoo na mbuzi, kitu chenye kuchukiza sana na wakati kitakaposimama mahali patakatifu, agano jipya, mgeuko-umbo, na ono la hekalu katika kitabu cha Ezekieli. Huenda nyakati nyingine ikawa vigumu kuelewa maelezo hayo yaliyorekebishwa, lakini sababu za maelezo hayo huwa wazi muda upitapo. Ikiwa Mkristo haelewi vizuri maelezo mapya juu ya andiko fulani, ni vema ayarudie kwa unyenyekevu maneno ya nabii Mika: “Nitamngojea Mungu wa wokovu wangu.”—Mika 7:7.

      19. Mabaki watiwa-mafuta na waandamani wao wa kondoo wengine wameonyeshaje ujasiri kama wa simba katika siku hizi za mwisho?

      19 Kumbuka kwamba mlinzi “[alilia] kama simba, Ee Bwana, mimi nasimama daima juu ya mnara wakati wa mchana, na kila usiku ninakaa katika zamu ya ulinzi wangu.” (Isaya 21:8) Mabaki watiwa-mafuta wamedhihirisha moyo mkuu kama wa simba katika kufichua dini isiyo ya kweli na kuonyesha watu njia iendayo kwenye uhuru. (Ufunuo 18:2-5) Wakiwa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” wameandaa Biblia, magazeti, na vichapo vinginevyo katika lugha nyingi—‘chakula kwa wakati ufaao.’ (Mathayo 24:45) Wameongoza katika kukusanya “umati mkubwa . . . kutoka katika mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na lugha.” Umati huo pia hutakaswa kwa damu ya Yesu yenye kufidi nao pia ni jasiri kama simba katika kumtolea Mungu “utumishi mtakatifu mchana na usiku.” (Ufunuo 7:9, 14, 15) Kikundi kidogo kinachosalia cha Mashahidi watiwa-mafuta wa Yehova na waandamani wao wa umati mkubwa kimepata matunda gani mwaka uliopita? Makala yetu inayofuata itatueleza.

  • Kutumikia Pamoja na Mlinzi
    Mnara wa Mlinzi—2000 | Januari 1
    • 19. Mabaki watiwa-mafuta na waandamani wao wa kondoo wengine wameonyeshaje ujasiri kama wa simba katika siku hizi za mwisho?

      19 Kumbuka kwamba mlinzi “[alilia] kama simba, Ee Bwana, mimi nasimama daima juu ya mnara wakati wa mchana, na kila usiku ninakaa katika zamu ya ulinzi wangu.” (Isaya 21:8) Mabaki watiwa-mafuta wamedhihirisha moyo mkuu kama wa simba katika kufichua dini isiyo ya kweli na kuonyesha watu njia iendayo kwenye uhuru. (Ufunuo 18:2-5) Wakiwa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” wameandaa Biblia, magazeti, na vichapo vinginevyo katika lugha nyingi—‘chakula kwa wakati ufaao.’ (Mathayo 24:45) Wameongoza katika kukusanya “umati mkubwa . . . kutoka katika mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na lugha.” Umati huo pia hutakaswa kwa damu ya Yesu yenye kufidi nao pia ni jasiri kama simba katika kumtolea Mungu “utumishi mtakatifu mchana na usiku.” (Ufunuo 7:9, 14, 15)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki