Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wakati wa Kutahini (1914-1918)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 69]

      ‘Hakuna Wanadamu Duniani Waliopendelewa Zaidi’

      Juni 21, 1918, J. F. Rutherford na washirika wake kadhaa wa karibu walihukumiwa kifungo cha miaka 20, wakiwa wamepatikana na hatia bandia ya kufanya njama. Hisia zao zilikuwa nini? Katika barua iliyoandikwa kwa mkono yenye tarehe ya Juni 22-23 (inayoonyeshwa chini), akiwa katika jela kwenye Raymond Street katika Brooklyn, New York, Ndugu Rutherford aliandika: “Labda hakuna wanadamu duniani leo waliopendelewa zaidi na walio na furaha zaidi ya wale ndugu saba walio gerezani sasa. Wao wanajua hawana hatia kabisa ya kosa la kukusudia, na washangilia kuwa wakiteseka pamoja na Kristo kwa ajili ya kumtumikia Yeye kwa uaminifu-mshikamanifu.”

  • Wakati wa Kutahini (1914-1918)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Picha katika ukurasa wa 69]

      Jela katika Raymond Street, katika Brooklyn, New York, ambamo Ndugu Rutherford na washirika wake kadhaa wa karibu walifungiwa kwa siku saba mara tu baada ya kuhukumiwa kwao

  • Wakati wa Kutahini (1914-1918)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Katika masika ya 1918, wimbi la mnyanyaso lilianzishwa dhidi ya Wanafunzi wa Biblia katika Amerika Kaskazini na Ulaya pia. Upinzani huo wenye kuchochewa na makasisi ulifikia upeo katika Mei 7, 1918, wakati waranti za serikali ya muungano ya Marekani zilipotolewa ili kukamata J. F. Rutherford na washirika wake kadhaa wa karibu. Kufikia katikati ya 1918, Rutherford na washirika saba walijipata wakiwa katika gereza la serikali ya muungano katika Atlanta, Georgia.

      Lakini Jaji Rutherford na washirika wake wakiwa gerezani, ni nini lililoupata utendaji kwenye makao makuu?

      Kuendeleza Kazi Bila Ndugu Wenye Madaraka

      Katika Brooklyn, Halmashauri ya Utekelezi iliwekwa ili kuchukua usimamizi wa kazi. Hangaiko kuu la ndugu waliowekwa lilikuwa kuendeleza mwenezo wa The Watch Tower. Hakika Wanafunzi wa Biblia kila mahali walihitaji kitia-moyo cha kiroho chote ambacho wangeweza kupewa. Kwa kweli, muda huo wote wa “majira ya kutahini,” hakuna toleo hata moja la The Watch Tower lililokosa kutokea katika chapa!f

      Hali ilikuwaje katika makao makuu? Thomas (Bud) Sullivan ambaye baadaye alitumikia akiwa mshiriki wa Baraza Linaloongoza, alikumbuka hivi: “Lilikuwa pendeleo langu kuzuru Betheli ya Brooklyn mwishoni-mwishoni mwa kiangazi cha 1918 wakati ndugu walipokuwa kifungoni. Ndugu waliosimamia kazi kwenye Betheli hawakuwa wenye woga wala wenye huzuni hata kidogo. Kwa kweli, hali ilikuwa kinyume kabisa. Walikuwa na maoni ya kutazamia mazuri na wenye uhakika kwamba hatimaye Yehova angewapa watu wake ushindi. Nilipendelewa kuwa penye meza ya kiamshakinywa Jumatatu asubuhi wakati ndugu waliokuwa wametumwa nje katika migawo ya mwisho-juma walipotoa ripoti zao. Kulikuwa hali nzuri. Katika kila kisa ndugu walikuwa na uhakika, wakimngojea Yehova aelekeze zaidi shughuli zao.”

      Hata hivyo, matatizo mengi yalikabiliwa. Vita ya Ulimwengu 1 ilikuwa ingali inachacha. Kulikuwa upungufu wa karatasi na makaa-mawe, vilivyohitajiwa sana kwa ajili ya kazi katika makao makuu. Uzalendo ukiwa unapamba moto, kulikuwa uhasama mwingi kuelekea Sosaiti; Wanafunzi wa Biblia walionwa kuwa wasaliti. Chini ya hali hizo kali, ilionekana kwamba haiwezekani kuendeleza shughuli za kazi katika Brooklyn. Kwa hiyo, baada ya kushauriana na ndugu wengine, Halmashauri ya Utekelezi iliuza Brooklyn Tabernacle na kufunga Kao la Betheli. Katika Agosti 26, 1918, shughuli za kazi zilihamishwa kurudi Pittsburgh kwenye jengo la ofisi katika barabara za Federal na Reliance.

      Hata hivyo, kulikuwa na hali changamfu. Martha Meredith alikumbuka hivi: “Sisi tuliokuwa katika Pittsburgh tulikusanyika na kuamua kwamba tungeendelea na kazi mpaka ndugu watoke gerezani. Katika wakati huo ofisi ya Brooklyn ilihamishiwa Pittsburgh, kwa hiyo ndugu walijishughulisha kuandika makala kwa ajili ya The Watch Tower na kuhakikisha kwamba zimechapwa. Magazeti ya The Watch Tower yalipokuwa tayari kupelekwa nje, sisi akina dada tuliyafunga na kuyapeleka nje kwa watu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki