Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Usitawi wa Muundo wa Tengenezo
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Mwaka huohuo ambao utumishi wa kolpota ulianza, Ndugu Russell alichapisha idadi fulani ya trakti (au vijitabu) vigawanywe bila malipo. Chenye kutokeza miongoni mwazo kilikuwa kile kijitabu Food for Thinking Christians, kilichogawanywa kufikia idadi ya nakala 1,200,000 katika miezi minne ya kwanza. Kazi iliyohusika katika kupanga uchapaji na ugawanyaji huo ndiyo iliyosababisha kufanyizwa kwa Zion’s Watch Tower Tract Society ili kuangalia mambo ya muhimu. Kuzuia kukatizwa kwa kazi ikiwa kifo chake chatukia, na ili kurahisisha kushughulikiwa kwa michango ipaswayo kutumiwa katika kazi, Ndugu Russell aliomba Sosaiti isajiliwe kisheria, na jambo hilo lilitiwa katika rekodi Desemba 15, 1884. Jambo hilo lilitokeza chombo cha kisheria kilichohitajiwa.

      Uhitaji ulipozuka, ofisi za tawi za Watch Tower Society zilianzishwa katika nchi nyinginezo. Ya kwanza ilikuwa katika London, Uingereza, katika Aprili 23, 1900. Nyingine, katika Elberfeld, Ujerumani, katika 1902. Miaka miwili baadaye, kwenye ule upande mwingine wa dunia, tawi lilipangwa kitengenezo katika Melbourne, Australia. Wakati wa kuandika kitabu hiki, kuna matawi 99 ulimwenguni pote.

      Ijapokuwa mipango ya kitengenezo iliyohitajiwa ili kutayarisha kiasi kikubwa cha fasihi ya Biblia ilikuwa ikisitawishwa, mwanzoni makutaniko yaliachwa yafanye mipango yao ya kugawanya hadharani habari hiyo.

  • Usitawi wa Muundo wa Tengenezo
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Toleo la Machi 1, 1917, la The Watch Tower lilitangaza kwamba, kuanzia hapo na kuendelea, ofisi ya Sosaiti itakuwa ikiwagawia makolpota na wafanyakazi wa uchungajie katika makutaniko maeneo yote ya kufanyia kazi. Mahali palipokuwa na wafanyakazi wenyeji na makolpota pia wakishiriki katika utumishi kama huo wa shambani katika jiji au wilaya, eneo liligawanywa miongoni mwao na halmashauri ya wilaya ya mahali iliyowekwa. Mpango huo ulichangia ugawanyaji wenye kutokeza kikweli wa The Finished Mystery katika muda wa miezi michache tu katika 1917-1918. Mpango huo ulikuwa wenye thamani pia katika kupata ugawanyaji wa kasi wa nakala 10,000,000 za ufichuo wenye nguvu wa Jumuiya ya Wakristo katika trakti iliyozungumzia habari “Kuanguka kwa Babiloni.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki