-
Afrika Kusini2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
BADILIKO LAFAIDI HUDUMA
Baraza Linaloongoza lilitoa mwongozo kwamba kuanzia mwaka wa 2000, makutaniko yote nchini Afrika Kusini yangeanza kutoa vichapo bila malipo kwa watu wote wanaopendezwa kikweli. Wahubiri wangewaalika watu kutoa michango kidogo kwa ajili ya kazi ya kuhubiri ya ulimwenguni pote.
Mpango huo wa kutoa michango ya hiari umewafaidi akina ndugu pamoja na wale wanaohubiriwa. Awali, wengi hawakuweza kugharimia vichapo vinavyotumiwa kwa ajili ya Funzo la Mnara wa Mlinzi na Funzo la Kitabu la Kutaniko. Katika makutaniko fulani yenye wahubiri 100, wahubiri kama 10 tu ndio waliokuwa na nakala za Mnara wa Mlinzi. Sasa kila mtu anaweza kupata nakala yake mwenyewe.
-
-
Afrika Kusini2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Tangu mpango wa kutoa vichapo bila malipo uanzishwe, vichapo vingi vinaagizwa. Idadi ya magazeti yanayochapishwa nchini Afrika Kusini imeongezeka kutoka milioni moja hadi milioni 4.4 kila mwezi. Maagizo ya vichapo yameongezeka kufikia tani 3,800 kila mwaka, ikilinganishwa na tani 200 mwaka wa 1999.
-