Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Unashiriki Katika Kufanya Mikutano ya Kikristo Iwe Yenye Kujenga?
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Oktoba 15
    • Kwa hiyo, kabla ya maandiko hayo kusomwa kwa sauti, yule anayeongoza mkutano huo anapaswa kuwapa wahudhuriaji wote wakati wa kutosha kufungua maandiko hayo na kufuata usomaji wa mistari hiyo.

  • Je, Unashiriki Katika Kufanya Mikutano ya Kikristo Iwe Yenye Kujenga?
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Oktoba 15
    • Muda fulani unapaswa kutumiwa kuzungumzia picha zilizo katika gazeti.—Soma Zaburi 22:22; 35:18; 40:9.

      8, 9. Kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi ana daraka gani?

      8 Hata hivyo, tutakuwa na wakati zaidi wa kutoa maelezo mbalimbali ikiwa tu washiriki wanatoa maelezo mafupi na yule anayeongoza mkutano huo anaepuka kutoa-toa maelezo kila wakati katika Funzo la Mnara wa Mlinzi. Hivyo basi, ni nini kinachoweza kumsaidia kiongozi awe na usawaziko unaofaa anapotoa maelezo yake na kutaniko linapotoa maelezo ili mkutano uwajenge watu wote?

      9 Ili kujibu swali hilo, fikiria mfano ufuatao. Funzo la Mnara wa Mlinzi ambalo linaongozwa vizuri ni kama shada au fungu la maua ambalo linavutia macho. Kama vile ambavyo fungu kubwa la maua linavyotengenezwa kutokana na maua mengi tofauti-tofauti, ndivyo Funzo la Mnara wa Mlinzi linavyofanyizwa na maelezo mengi tofauti-tofauti. Na kama vile tu ambavyo ua moja katika fungu hilo lilivyo na ukubwa na rangi tofauti na maua mengine, ndivyo maelezo yanayotolewa kwenye mkutano yanavyotofautiana katika urefu na jinsi yanavyotolewa. Kiongozi wa funzo hilo ana daraka gani? Maelezo yake ya mara moja moja ni kama mimea michache ya kijani-kibichi ambayo inaongezwa kwa uangalifu kwenye fungu la maua. Mimea hiyo michache haitawali; badala yake, inasaidia kuboresha na kuunganisha fungu lote la maua. Vivyo hivyo, yule anayeongoza anahitaji kukumbuka kwamba daraka lake si kutawala mazungumzo, bali ni kukamilisha maelezo ya kumsifu Mungu ambayo yanatolewa na kutaniko. Ndiyo, maelezo mengi mbalimbali yanayotolewa na kutaniko yakiunganishwa kwa ustadi na maelezo machache yanayotolewa wakati unaofaa na yule anayeongoza, yanakuwa kama fungu maridadi la maneno ambalo litawavutia wote wanaohudhuria.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki