-
Jua Jinsi Unavyopaswa KujibuFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
Kutoa Maelezo Katika Mikutano ya Kutaniko
Mara nyingi mikutano ya kutaniko la Kikristo huandaa fursa za kutangaza imani yetu mbele ya watu. Njia mojawapo ya kufanya hivyo ni kutoa maelezo kwa kujibu maswali. Tutoeje maelezo? Tukiwa na tamaa ya kumbariki Yehova, au kusema mema juu yake. Ndivyo alivyofanya mtunga-zaburi Daudi alipokuwa katika “makusanyiko.” (Zab. 26:12) Pia tutoe maelezo kwa njia inayowatia moyo waamini wenzetu, tukiwachochea “kwenye upendo na kazi zilizo bora,” kama mtume Paulo alivyohimiza. (Ebr. 10:23-25) Kujifunza mapema masomo hayo kunaweza kutusaidia kutimiza jambo hilo.
Unapoombwa kutoa maelezo, toa maelezo rahisi, ya wazi, na mafupi. Usizungumzie fungu lote; zungumzia jambo moja tu. Ukitoa sehemu tu ya jibu, wengine pia watapata fursa ya kutoa maelezo ya ziada. Ni jambo lenye faida hasa kutaja maandiko ambayo yameonyeshwa katika habari hiyo. Unapofanya hivyo, jaribu kukazia sehemu ya andiko hilo inayohusu jambo linalozungumziwa. Jifunze kutoa maelezo yako mwenyewe badala ya kusoma fungu moja kwa moja. Usifadhaike kama maelezo yako hayatokei vizuri sana. Kila mmoja anayetoa maelezo hupatwa na hali hiyo mara kwa mara.
-