-
Unaalikwa kwa UchangamfuMnara wa Mlinzi—2009 | Februari 1
-
-
Funzo la Mnara wa Mlinzi
Katika makutaniko mengi ya Mashahidi wa Yehova, hotuba ya watu wote inafuatwa na Funzo la Mnara wa Mlinzi ambalo ni mazungumzo ya saa moja ya maswali na majibu juu ya kichwa fulani cha Biblia. Mkutano huo unawatia moyo wote waliohudhuria wafuate mfano wa Waberoya walioishi katika siku za Paulo ambao “walilipokea neno kwa hamu kubwa zaidi ya akili, wakiyachunguza Maandiko kwa uangalifu.”—Matendo 17:11.
Funzo la Mnara wa Mlinzi linaanza kwa wimbo. Habari inayozungumziwa na maswali ambayo yanaulizwa na yule anayeongoza yanapatikana katika toleo la funzo la gazeti hili. Unaweza kupata nakala ya toleo la funzo kutoka kwa Shahidi wa Yehova. Vichwa ambavyo vimezungumziwa hivi karibuni vinatia ndani: “Wazazi—Wazoezeni Watoto Wenu Kwa Upendo,” “Msimlipe Yeyote Uovu Kwa Uovu,” na “Sababu Kwa Nini Mateso Yote Yatakwisha Karibuni.” Ingawa mkutano huo unaongozwa kwa maswali na majibu, wasikilizaji wanatoa maelezo kwa hiari na wale wanatoa maelezo huwa wamesoma na kufikiria kuhusu habari hiyo mapema na kusoma maandiko yaliyopo. Mkutano huo unaisha kwa wimbo na sala.—Mathayo 26:30; Waefeso 5:19.
-
-
Unaalikwa kwa UchangamfuMnara wa Mlinzi—2009 | Februari 1
-
-
[Picha katika ukurasa wa 21]
Funzo la “Mnara wa Mlinzi”
-