-
Maji—Uhai wa SayariAmkeni!—1997 | Agosti 22
-
-
Kwa uzuri, kuna maji tele. Ipigwapo picha kutoka anga za nje, sayari yetu maridadi ya buluu huonekana kana kwamba yapasa kuitwa Maji, si Dunia. Kwa hakika, ikiwa maji ya ulimwengu yangefunika kwa usawa uso wa sayari, yangefanyiza bahari-kuu ya tufeni pote yenye kina cha kilometa 2.5. Mabara yote ya dunia yangetoshea katika Bahari-Kuu ya Pasifiki, na nafasi ibaki.
-
-
Maji—Uhai wa SayariAmkeni!—1997 | Agosti 22
-
-
Kwa msingi, kiwango cha jumla cha maji duniani hakiongezeki wala hakipungui. Gazeti Science World lataarifu: “Maji unayoyatumia leo huenda wakati mmoja yalizima kiu cha dinosau. Hiyo ni kwa sababu maji yote tuliyo nayo Duniani sasa ndiyo yote ambayo tumepata kuwa nayo—au tutakayopata kuwa nayo.”
Hii ni kwa sababu maji yaliyo ndani na yanayozunguka ulimwengu huzunguka bila kikomo—kutoka baharini hadi angahewa, hadi barani, kuingia mitoni, na kurudi baharini tena. Ni kama vile yule mwanamume mwenye hekima alivyoandika zamani za kale: “Vijito vyote huingia baharini, hata hivyo bahari haifuriki kamwe; mahali ambapo vijito vilitoka hivyo hurudi ili vitoke tena.”—Mhubiri 1:7, New English Bible.
-