-
Sehemu Zenye Shida ZaidiAmkeni!—1997 | Agosti 22
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 9]
Kile Ambacho Kimependekezwa
Kujenga viwanda vya kuondoa chumvi. Hivi huondoa chumvi kutoka katika maji ya bahari. Hilo kwa kawaida hufanywa kwa kupiga pampu maji ndani ya vyumba vyenye msongo wa chini, ambapo maji huchemshwa. Maji huvukizika na kuelekezwa kwingine, yakiacha chembechembe za chumvi. Ni utaratibu wenye kugharimu sana, usioweza kufikiwa na nchi nyingi zinazoendelea.
Kuyeyusha vilima vya barafu. Wanasayansi fulani huamini kwamba vilima vya barafu vilivyo vikubwa sana, ambavyo vina maji safi na matamu, vyaweza kuburutwa kutoka Antaktika na meli kubwa za kuburuta ili viyeyushwe na kuandaa maji kwa nchi kame zilizo katika Kizio cha Kusini. Tatizo moja ni: Nusu hivi ya kila kilima cha barafu kitayeyuka baharini kabla ya kufika mahali kinapopelekwa.
Kuteka maji ya miamba-maji. Miamba-maji ni miamba iliyo chini sana ardhini yenye maji. Maji yaweza kupigwa pampu, hata katika jangwa kavu zaidi kutoka katika miamba hiyo. Lakini kuteka maji haya ni ghali na hushusha tabaka ya maji. Tatizo jingine ni: Miamba-maji mingi hurudia hali yake polepole—na mingine hairudii kabisa hali yake.
-
-
Suluhisho Ni Nini?Amkeni!—1997 | Agosti 22
-
-
WATAALAMU wana mijadala motomoto kuhusu masuluhisho ya matatizo tata ya maji ya wanadamu. Benki ya Ulimwengu yataka dola bilioni 600 zitumiwe kwa usafi wa kutunza afya na mipango ya maji kwa miaka kumi ijayo. Gharama ya kutotumia pesa hizo yaweza kuwa juu hata zaidi. Kwa mfano, nchini Peru, mweneo wa kipindupindu kwa majuma kumi, uliosababishwa na maji machafu, hivi majuzi uligharimu karibu dola bilioni 1—mara tatu ya fedha zilizotumiwa katika ugavi wa maji wa hiyo nchi katika mwongo wote wa miaka ya 1980.
Hata hivyo, japo makusudio mazuri ya wale wanaoiendeleza, miradi ya maji mara nyingi haisaidii sana wale walio maskini zaidi. Ongezeko katika majiji makubwa ya nchi zinazoendelea ni la haraka sana na la kiholela. Maskini huishi katika vibanda hafifu vilivyosongamana kupita kiasi na visivyo na maji au usafi wa kutunza afya. Kwa kuwa hawawezi kufikia huduma za maji zinazotolewa na serikali, ni lazima wanunue maji kwa bei ghali kutoka kwa watu binafsi, mara nyingi maji machafu.
Kwa wazi, shida ya maji tufeni pote ni tata na huhusisha visababishi vinavyohusiana: upungufu wa maji, uchafuzi, umaskini, maradhi, na uhitaji unaoongezeka wa idadi za watu zenye kuongozeka. Vivyo hivyo ni wazi kwamba wanadamu hawawezi kutatua matatizo haya.
-