Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Waadilifu Watang’aa kwa Uangavu Kama Jua”
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
    • 5. Adui anayetajwa katika mfano huo ni nani, na magugu yanafananisha nani?

      5 Adui ni nani, na magugu ni nani? Yesu anatuambia kwamba adui “ni Ibilisi.” Biblia inasema magugu ni “wana wa yule mwovu.” (Mt. 13:25, 38, 39) Kwa njia halisi, magugu ambayo Yesu alizungumzia huenda yalikuwa magugu fulani yenye sumu ambayo yanafanana sana na ngano ambayo haijakomaa. Mfano huo unawafaa sana Wakristo wa uwongo, wale wanaodai kuwa wana wa Ufalme lakini hawazai matunda yanayofaa! Wakristo hao wenye unafiki ambao wanadai kuwa wafuasi wa kweli wa Kristo kwa kweli wao ni sehemu ya “mbegu” ya Shetani Ibilisi.—Mwa. 3:15.

      6. Magugu yalianza kutokea wakati gani, na watu walikuwa “wamelala usingizi” jinsi gani wakati huo?

      6 Wakristo hao ambao ni kama magugu walitokea wakati gani? Yesu anasema hivi: “Watu wakiwa wamelala usingizi.” (Mt. 13:25) Ni wakati gani huo? Tunapata jibu katika maneno ambayo mtume Paulo aliwaambia wazee wa huko Efeso: “Ninajua kwamba baada ya kuondoka kwangu mbwa-mwitu wenye kukandamiza wataingia katikati yenu nao hawatalitendea kundi kwa wororo, na kutoka katikati yenu ninyi wenyewe watu watasimama na kusema mambo yaliyopotoka ili kuwavuta wanafunzi wawafuate wao wenyewe.” (Mdo. 20:29, 30) Kisha akawahimiza wazee hao wakae macho kiroho. Mitume, ambao walikuwa kama “kizuizi” kwa uasi-imani, walipoanza kulala usingizi katika kifo, Wakristo wengi walilala usingizi wa kiroho. (Soma 2 Wathesalonike 2:3, 6-8.) Uasi-imani mkubwa ulianza wakati huo.

      7. Je, ngano iligeuka na kuwa magugu? Eleza.

      7 Yesu hakusema kwamba ngano ingegeuka na kuwa magugu, alisema kwamba magugu yangepandwa katikati ya ngano. Kwa hiyo, mfano huo haumaanishi kwamba Wakristo wa kweli wangeacha kweli. Badala yake, unaonyesha kwamba Shetani angejitahidi kwa makusudi kulipotosha kutaniko la Kikristo kwa kuingiza watu waovu ndani yake. Mtume wa mwisho, Yohana, alipokuwa amezeeka, uasi-imani huo ulikuwa unaonekana waziwazi.—2 Pet. 2:1-3; 1 Yoh. 2:18.

      “Acheni Zikue Pamoja Mpaka Wakati wa Mavuno”

      8, 9. (a) Kwa nini wasikilizaji wa Yesu waliona hekima ya maagizo ambayo Bwana aliwapa watumwa wake? (b) Ngano na magugu ya mfano yalikua pamoja jinsi gani?

      8 Watumwa wanamwambia Bwana wao tatizo wanalokabili na kumuuliza hivi: “Basi, je, unataka twende kuyakusanya [magugu]?” (Mt. 13:27, 28) Huenda jibu lake likaonekana kuwa lenye kushangaza. Anawaambia waache ngano na magugu yakue pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wanafunzi wa Yesu wangeona hekima ya kutii amri hiyo. Walijua kwamba ni vigumu kutofautisha ngano na yale magugu yenye sumu yanayofanana kabisa na ngano. Wanafunzi waliojua mambo ya ukulima walitambua pia kwamba kwa kawaida mizizi ya magugu hayo inaingia katikati ya mizizi ya ngano.c Ndiyo sababu Bwana wao anawaambia wangoje!

      9 Vivyo hivyo, kwa karne nyingi, madhehebu mbalimbali ya dini zinazodai kuwa za Kikristo yamezaa magugu mengi sana, kwanza katika makanisa ya Kikatoliki na ya Kiothodoksi na baadaye katika vikundi vingi sana vya Kiprotestanti ambavyo vilisitawi.

  • “Waadilifu Watang’aa kwa Uangavu Kama Jua”
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
    • Katika siku za mwisho za mfumo huu mwovu wa mambo, wana wa Ufalme wanakusanywa na kutenganishwa kutoka kwa watu wowote ambao ni kama magugu. Mtume Petro anatuambia hivi kuhusu jambo hilo: “Ni wakati uliowekwa wa hukumu kuanza na nyumba ya Mungu. Sasa ikiwa inaanza na sisi kwanza, basi mwisho wa wale wasioitii habari njema ya Mungu utakuwaje?”—1 Pet. 4:17.

      11 Muda mfupi baada ya siku za mwisho au “umalizio wa mfumo wa mambo” kuanza, wale waliodai kuwa Wakristo wa kweli walianza kuhukumiwa ili kuamua ikiwa kwa kweli walikuwa “wana wa ufalme” au “wana wa yule mwovu.” “Kwanza” Babiloni Mkubwa alianguka, “ndipo” wana wa Ufalme wakakusanywa pamoja wakati kazi ya kuvuna ilipoanza. (Mt. 13:30)

  • “Waadilifu Watang’aa kwa Uangavu Kama Jua”
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
    • 13. Magugu yanasababisha kukwazika namna gani, nao wanaasi sheria jinsi gani?

      13 Ni nani watakaokusanywa kutoka katika Ufalme, na wanasababisha jinsi gani kukwazika na kuasi sheria? (Mt. 13:41) Viongozi wa dini zinazodai kuwa za Kikristo ambao ni kama magugu wamepotosha mamilioni ya watu kwa karne nyingi. Wamefanya hivyo kwa kufundisha mafundisho ambayo hayamletei Mungu heshima, ‘mambo ambayo yanasababisha kukwazika,’ kama vile fundisho la watu kuadhibiwa milele katika moto wa mateso na fundisho la Utatu ambalo ni fumbo lisiloeleweka. Viongozi wengi wa kidini wamewawekea mfano mbaya sana kondoo wao kwa kufanya uzinzi pamoja na ulimwengu huu na nyakati nyingine wanatenda waziwazi mambo yaliyopotoka kimaadili. (Yak. 4:4) Kwa kuongezea, dini zinazodai kuwa za Kikristo zinawaruhusu washiriki wake waendelee kuwa na mwenendo mpotovu wa kingono. (Soma Yuda 4.) Hata ingawa wanatenda mambo hayo yote, wanaendelea kujionyesha kwa nje kuwa watakatifu na watu wanaomwogopa Mungu. Wana wa Ufalme wanafurahi kama nini kutengwa mbali na uvutano huo wa magugu na mafundisho yenye kupotosha ambayo yanawakwaza watu!

      14. Watu ambao ni kama magugu wanalia na kusaga meno yao jinsi gani?

      14 Watu ambao ni kama magugu wanalia na kusaga meno yao jinsi gani? (Mt. 13:42) “Wana wa yule mwovu” wanateseka kwa sababu “wana wa ufalme” wamefunua hali ya kiroho yenye sumu ya magugu hayo ya mfano. Pia, wanaomboleza kwa sababu washiriki wengi wa makanisa yao hawaungi tena mkono dini, hivyo wanapoteza mamlaka ya kuwaongoza.—Soma Isaya 65:13, 14.

      15. Watu ambao ni kama magugu wanateketezwa kwa moto namna gani?

      15 Ni katika maana gani magugu yanakusanywa na kuteketezwa kwa moto? (Mt. 13:40) Hilo linaonyesha jambo ambalo litayapata magugu hayo mwishowe. Kutupwa kwa magugu hayo kwa njia ya mfano ndani ya tanuru ya moto kunaonyesha kwamba yataharibiwa milele. (Ufu. 20:14; 21:8) Wakristo wa uwongo na wadanganyifu ambao ni kama magugu, wataharibiwa kabisa wakati wa “dhiki kuu.”—Mt. 24:21.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki