Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Samoa
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Mwezi wa Januari, 1953, ibada ya kweli nchini Samoa ilipiga hatua kubwa. Kwa kuwa tayari watu 40 hivi walikuwa wakihudhuria mikutano kufikia wakati huo, ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova nchini Australia iliidhinisha kuundwa kwa kutaniko la kwanza nchini Samoa, katika mji wa Apia. Ndugu Croxford aliporudi Uingereza, Pele aliyekuwa amebatizwa karibuni akaanza kusimamia kutaniko.

  • Samoa
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Baada ya kupewa mahali pa kukaa na familia ya Pele, akina Sellars walianza kazi mara moja. “Nilipanga kukutana na akina ndugu kila jioni ili kuwajibu maswali yao mengi,” asema Ron. “Ijapokuwa walijua mafundisho ya msingi ya Biblia, muda si muda niliona kwamba wanahitaji kufanya mabadiliko mbalimbali ili kupatanisha maisha yao na viwango vya Mungu. Ili kuwasaidia kufanya hivyo, Dolly nami tulijitahidi sana kuwa na subira na kuwaonyesha upendo mwingi sana.” Hata hivyo, kwa kusikitisha, wengine walikataa marekebisho hayo ya upendo yaliyotokana na Maandiko na baada ya muda wakaacha kushirikiana na kutaniko. Lakini, wengine walikuwa wanyenyekevu nao walikubali mafundisho na mahimizo hayo. Baadaye, wakafanya maendeleo ya kiroho, na kwa sababu hiyo, kutaniko likasafishwa na kuimarishwa.

  • Samoa
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Baada ya muda fulani kikundi chetu kidogo kikawa kutaniko la pili nchini Samoa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki