-
Samoa2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Ane Ropati alikuwa na umri wa miaka 13 wazazi wake walipoacha kuhudhuria mikutano. Alikuwa akiwatayarisha ndugu zake wawili na dada yake mmoja na kutembea kilomita 8 hadi kwenye Jumba la Ufalme ili kuhudhuria mikutano. Baadaye akawa painia, naye alisaidia pia katika ujenzi wa ofisi ya tawi ya Siusega. “Wamishonari,” asema Ane, “walinichochea sana na kunisaidia kufanya maendeleo kiroho.” Wakati wa ujenzi, alikutana na Steve Gauld, mjitoleaji kutoka Australia. Walifunga ndoa na kutumikia wakiwa watumishi wa kimataifa katika miradi mbalimbali ya ujenzi barani Asia ya Kusini-Mashariki, Afrika, na Urusi kabla ya kurudi Betheli ya Samoa. Sasa wanatumikia katika ofisi ya tawi ya Australia.
-
-
Samoa2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 131]
Ane Ropati (anayeitwa Gauld sasa) alichukua msimamo wake upande wa Yehova akiwa kijana
-