-
Samoa2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Geoffrey Jackson, ambaye wakati huo alikuwa akitumikia katika ofisi ya tawi ya Samoa, alijaribu pasipo mafanikio kuwasiliana na kamishna wa New Zealand anayeshughulikia masuala ya Tokelau ili ajadiliane naye kuhusu matatizo ambayo Mashahidi wa Yehova wanakumbana nayo katika visiwa hivyo. “Hata hivyo, nilipewa kibali cha kuzuru Tokelau kama mwana-isimu,” asema Geoff, “na tukiwa safarini, kapteni wa meli hiyo alinikaribisha nijiunge naye pamoja na mwanamume mwingine katika sebule ya maofisa wa meli ili kupata kinywaji. Kumbe mwanamume huyo ndiye yuleyule kamishna wa masuala ya Tokelau ambaye tulikuwa tukijaribu kuwasiliana naye! Tulizungumza kwa zaidi ya saa nzima. Mwishoni mwa mazungumzo yetu, alinishukuru na kuahidi kwamba atafanya kila awezalo ili kuwasaidia ndugu zetu walio Tokelau.”
-
-
Samoa2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
KAZI YA KUTAFSIRI YAPAMBA MOTO
Kadiri idadi ya wahubiri ilivyoongezeka, ndivyo pia uhitaji wa vitabu katika lugha ya Kisamoa ulivyoongezeka. Ili kutosheleza uhitaji huo, mwaka wa 1985, Geoffrey Jackson na mke wake, Jenny, walihamishwa kutoka Tuvalu, walipokuwa wakitumikia wakiwa wamishonari, na kwenda katika ofisi ya tawi ya Samoa. Geoff alipewa mgawo wa kusimamia timu yenye watafsiri wawili. “Mwanzoni,” anasema, “watafsiri walitumia meza zilizokuwa katika chumba cha kulia cha Betheli. Kila asubuhi, waliondoa vyombo mezani baada ya kiamsha-kinywa kabla ya kuanza kutafsiri. Kisha, kabla tu ya chakula cha mchana, waliondoa vifaa vyao na kutayarisha meza kwa ajili ya chakula cha mchana. Tena, baada ya chakula, waliondoa vyombo mezani na kuendelea na kazi yao.”
Shughuli hizo ziliathiri sana kazi yao. Kazi ya kutafsiri ilikuwa ngumu nayo ilichukua wakati mwingi. “Mara nyingi waliandika tafsiri zao kwa mkono kisha kuzichapa,” akumbuka Geoff. “Kila karatasi ilichapwa mara kadhaa, ili kufanyiwa masahihisho, kabla ya kuwa tayari kuchapishwa.”
-
-
Samoa2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
“Kutolewa kwa Amkeni!” akumbuka Geoff, “kulitangazwa, si katika magazeti ya kilimwengu na redio tu lakini pia kupitia televisheni.”
-