-
Samoa2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
John Rhodes, ambaye kwa miaka 20 alikuwa mmishonari nchini Samoa na Samoa ya Marekani anasema: “Wenye nyumba walitukaribisha na kusema kwamba tumewaonyesha heshima kubwa kwa kuwapelekea ujumbe wa Biblia katika nyumba zao duni. Kisha wangetusalimu kwa kutuuliza maswali kama vile: Mmetoka wapi? Mna watoto? Kwenu ni wapi?”
Helen, mke wa John, anasema: “Sikuzote tulizungumza na wenye nyumba tukitumia maneno ya heshima ambayo kwa kawaida yalitumiwa wakati wa pindi rasmi. Kufanya hivyo kulionyesha kwamba tunamheshimu mwenye nyumba na kuufanya ujumbe wetu wa Biblia uheshimiwe.”
-
-
Samoa2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
John Rhodes anasema: “Kiasili, Wasamoa huzungumza kwa ufasaha, na wapya wengi wangeweza kuzungumza na wengine kuhusu imani yao kwa usadikisho hata pasipo mazoezi mengi. Hata hivyo, tuliwatia moyo watumie mapendekezo yaliyochapishwa na kujadiliana na watu kwa kutumia Maandiko badala ya kutegemea tu uwezo wao wa kiasili wa kusema.”
-