-
Ukweli Kuhusu Uchawi na UloziJe, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?
-
-
10. Ni nini ambacho husemwa kuwahusu wachawi, na tunajuaje kwamba huo ni uwongo?
10 Uwongo wa pili ambao Shetani huendeleza ni huu: Wachawi wanaweza kubadilika au kubadilishwa kuwa wanyama ili kuwadhuru wengine. Hebu jiulize: ‘Ikiwa wachawi wanaweza kufanya hivyo, ni nini hasa hutoka katika mwili na kuingia ndani ya mwili wa mnyama?’ Kama tulivyoona, roho si kitu kinachoweza kuuacha mwili wa mtu. Roho ni nguvu ya uhai ambayo huutia mwili nguvu lakini haiwezi kufanya chochote bila mwili. Kubadilika na kuwa mnyama ni kinyume cha sheria za maumbile zilizoanzishwa na Yehova Mungu. Bila shaka, Mungu hangepuuza sheria zake kwa kuwapa wanadamu uwezo wa kujibadili na kuwa wanyama wasio na akili.
11. Tunajuaje kwamba wachawi hawawezi kuiacha miili yao au kujibadili kuwa wanyama, na je, wewe unaamini hilo?
11 Roho haiwezi kuuacha mwili na kwenda kufanya jambo lolote baya au zuri. Hivyo, wachawi hawawezi kuiacha miili yao au kujibadili kuwa wanyama. Kwa kweli hawafanyi mambo wanayodai au wanayofikiri wamefanya.
12. Ni kwa njia gani Shetani huwafanya watu waamini kwamba wamefanya mambo ambayo hawakufanya?
12 Tunaweza kuelezaje mambo ambayo wale waliokuwa wachawi wanakiri kwamba walifanya? Shetani anaweza kufanya watu waamini kwamba wameona mambo ambayo hawakuona. Kupitia maono, Shetani anaweza kufanya watu wafikiri kwamba wameona, kusikia, au kufanya mambo ambayo hawakufanya. Kwa njia hiyo, Shetani anatarajia kugeuza watu wamwache Yehova na kuwafanya wafikiri kwamba Biblia si ya kweli.
-
-
Ukweli Kuhusu Uchawi na UloziJe, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?
-
-
Uwongo na Udanganyifu
6. Shetani na roho wake waovu walifanya nini zamani, nasi tunapaswa kuzionaje nguvu zao?
6 Ni kweli kwamba Shetani na roho wake waovu ni maadui hatari wa wanadamu. Wana nguvu za kudhibiti akili na maisha ya watu, na zamani hata waliwapagaa wanadamu na wanyama. (Mathayo 12:43-45) Ingawa hatupaswi kupuuza nguvu zao, hatupaswi pia kuziona kuwa kubwa mno.
7. Shetani anataka tuamini nini, na ni mfano gani unaoonyesha jambo hilo?
7 Shetani ni mdanganyifu stadi. Yeye huwapumbaza watu wafikiri kwamba ana nguvu nyingi kuliko ilivyo kwa kweli. Kwa mfano: Wakati wa vita vya hivi karibuni katika nchi moja ya Afrika, askari-jeshi walitumia vikuza sauti ili kuwaogopesha maadui wao. Kabla ya kushambulia, askari hao walikuwa wakivumisha mlio mkubwa wa mizinga na bunduki uliokuwa umerekodiwa. Walitaka maadui wao wafikiri kwamba wanashambuliwa na jeshi lenye silaha nzito-nzito. Kwa njia hiyohiyo, Shetani hutaka watu waamini kwamba ana nguvu kubwa mno. Kusudi lake ni kuogopesha watu wasifanye mapenzi ya Yehova bali wafanye mapenzi yake. Na tuone aina tatu za uwongo ambao Shetani hutaka watu waamini.
8. Ni uwongo gani ambao Shetani huendeleza?
8 Uwongo mmoja ambao Shetani huendeleza ni huu: Hakuna jambo lolote baya linalotukia tu; kila jambo baya husababishwa na mtu fulani au na nguvu zisizo za kawaida. Kwa mfano, tuseme mtoto amekufa kwa ugonjwa wa malaria. Huenda mama yake anajua kwamba malaria ni ugonjwa ambao huenezwa na mbu. Lakini huenda pia akaamini kwamba mtu fulani alitumia uchawi kutuma mbu aje kumwuma mtoto wake.
9. Biblia inaonyeshaje kwamba Shetani hasababishi kila tatizo?
9 Ingawa Shetani ana nguvu za kusababisha matatizo fulani, ni kosa kuamini kwamba ana nguvu za kusababisha kila tatizo. Biblia inasema: “Si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini wakati na bahati [“tukio lisilotazamiwa,” NW] huwapata wote.” (Mhubiri 9:11) Mkimbiaji mmoja anaweza kukimbia kwa kasi kushinda wengine, lakini asishinde. ‘Tukio fulani lisilotazamiwa’ linaweza kumfanya asishinde. Labda anajikwaa na kuanguka au anapatwa na tatizo la misuli. Mambo hayo yanaweza kumpata yeyote. Si lazima yawe yanasababishwa na Shetani au uchawi; yanatukia tu.
-
-
Ukweli Kuhusu Uchawi na UloziJe, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?
-
-
13. (a) Je, uchawi unaoaminiwa kuleta ulinzi unafaa? (b) Biblia inasema nini kuhusu uchawi?
13 Uwongo wa tatu ni huu: Uchawi unaoaminiwa kutoa ulinzi unafaa kwa kuwa inaaminika kwamba unaweza kuumaliza nguvu ule uchawi unaodhuru. Biblia haitofautishi kati ya uchawi unaotoa ulinzi na uchawi unaodhuru. Inashutumu uchawi wa aina zote. Ona sheria ambazo Yehova alipatia taifa la Israeli kuhusu uchawi na wale wanaoutumia:
● ‘Msifanye uchawi.’—Mambo ya Walawi 19:26, Biblia Habari Njema.
● “Mtu mume au mtu mke aliye na pepo, au aliye mchawi, hakika atauawa.”—Mambo ya Walawi 20:27.
● “Asionekane kwako . . . mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri, wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi.”—Kumbukumbu la Torati 18:10-14.
14. Kwa nini Yehova alitunga sheria za kupinga uchawi?
14 Sheria hizo zinaonyesha wazi kwamba Mungu hakutaka watu wake wawe wachawi. Yehova aliwapa watu wake sheria hizo kwa sababu aliwapenda na hakutaka wawe watumwa wa woga na ushirikina. Hakutaka wakandamizwe na roho waovu.
15. Biblia inaonyeshaje kwamba Yehova ana nguvu nyingi zaidi kuliko Shetani?
15 Ingawa Biblia haizungumzii kwa undani mambo ambayo roho waovu wanaweza kufanya na wasiyoweza kufanya, inaonyesha kwamba Yehova Mungu ana nguvu nyingi zaidi kuliko Shetani na roho wake waovu. Yehova alimfanya Shetani atupwe kutoka mbinguni. (Ufunuo 12:9) Ona pia kwamba Shetani aliomba ruhusa ya kumjaribu Yobu naye alitii amri ya Mungu ya kutomwua Yobu.—Ayubu 2:4-6.
16. Tunapaswa kumtegemea nani atulinde?
16 Andiko la Mithali 18:10 linasema: “Jina la BWANA ni ngome imara; mwenye haki huikimbilia, akawa salama.” Hivyo tunapaswa kumtegemea Yehova atulinde. Watumishi wa Mungu hawategemei hirizi au dawa za uchawi ziwalinde dhidi ya matendo maovu ya Shetani na roho wake waovu, wala hawaogopi walozi. Watumishi wa Mungu huamini yale ambayo Biblia inasema: “Macho ya BWANA hukimbia-kimbia duniani mwote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao, waliokamilika moyo kuelekea kwake.”—2 Mambo ya Nyakati 16:9.
17. Andiko la Yakobo 4:7 linatuhakikishia nini, lakini tunapaswa kufanya nini?
17 Wewe pia unaweza kuwa na uhakika huo ikiwa unamtumikia Yehova. Andiko la Yakobo 4:7 linasema: “Jitiisheni wenyewe kwa Mungu; lakini mpingeni Ibilisi, naye atawakimbia.” Ikiwa unamtumikia Mungu wa kweli na kujitiisha kwake, unaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atakulinda.
-