Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kwa Nini Tufanye Kazi?
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
    • Yesu alipokuwa duniani, hakufanya useremala maisha yake yote. Yehova Mungu alimpa kazi ya pekee duniani. Unajua ni kazi gani?— Yesu alisema: ‘Lazima nitangaze habari njema ya ufalme wa Mungu, kwa sababu nilitumwa kufanya hivyo.’ (Luka 4:43) Wakati mwingine Yesu alipowahubiria watu, walimwamini na wakawaambia wengine waliyosikia, kama alivyofanya mwanamke huyu Msamaria unayemwona kwenye picha.—Yohana 4:7-15, 27-30.

      Yesu aliionaje kazi hiyo? Unafikiri alitaka kuifanya?— Yesu alisema: ‘Chakula changu ni kufanya mapenzi yake aliyenituma na kuimaliza kazi yake.’ (Yohana 4:34) Wewe hufurahia kula chakula ukipendacho kadiri gani?— Basi unaweza kuelewa jinsi Yesu alivyofurahia kufanya kazi aliyopewa na Mungu.

  • Kwa Nini Tufanye Kazi?
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
    • Mwalimu Mkuu alifurahia kuona watoto wakicheza. Kabla ya kuja duniani, alisema: “Ndipo nilipokuwa kando yake [Mungu] nikiwa stadi wa kazi . . . nikifurahi mbele zake wakati wote.” Ona kwamba Yesu alifanya kazi pamoja na Yehova mbinguni. Na alipokuwa huko alisema: “Vitu nilivyopenda sana vilihusiana na wana wa binadamu.” Ndiyo, kama tulivyojifunza hapo awali, Mwalimu Mkuu alipendezwa kikweli na kila mtu, kutia ndani watoto.—Mithali 8:30, 31.

      Unafikiri Yesu alicheza alipokuwa mtoto?— Labda. Lakini kwa sababu alikuwa “stadi wa kazi” mbinguni, je, alifanya kazi duniani pia?— Yesu aliitwa ‘mwana wa seremala.’ Lakini aliitwa pia “seremala.” Hii inamaanisha nini?— Ni lazima Yosefu, baba-mlezi wa Yesu, alimfundisha useremala. Basi Yesu akawa seremala pia.—Mathayo 13:55; Marko 6:3.

      Yesu alikuwa seremala wa aina gani?— Kwa sababu alikuwa stadi wa kazi mbinguni, je, si wazi pia kwamba alikuwa seremala stadi duniani?— Ona jinsi ilivyokuwa kazi ngumu kuwa seremala wakati huo. Huenda Yesu alilazimika kuukata mti, kuupasua vipande-vipande, kubeba mbao zake na kuzipeleka nyumbani, kisha akatengeneza meza, benchi, na vitu vinginevyo.

      Unafikiri Yesu alifurahia kazi hiyo?— Je, ungefurahi ikiwa ungetengeneza meza nzuri na viti vizuri na vitu vingine ili vitumiwe?— Biblia inasema ni vizuri mtu “afurahie kazi zake.” Kazi huleta shangwe ambayo huwezi kupata katika mchezo.—Mhubiri 3:22.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki