Je, Mwaka wa 1914 Ni Mwanzo wa Karne ya 20?
“Karne ya 19—iliyofafanuliwa kuwa itikadi, makisio, mitazamo, na maadili—haikumalizika Jan[uari] 1, 1901,” akaandika mwandishi wa magazeti Charley Reese. “Iliisha mwaka wa 1914. Huo ndio wakati pia ambapo karne ya 20, kwa maana ileile, ilipoanza.”
Reese aeleza: “Yaelekea kwamba mahitilafiano yote ambayo yametuhangaisha muda wote wa maisha yetu yalitokana na vita hiyo [ya kwanza ya ulimwengu]. . . . Ilivunjavunja matazamio mema katika karne ya 19 na kutokeza dhana mpya katika karne ya 20 za kutanguliza anasa maishani, kutojali watu, mahangaiko, hofu na ukataaji wa mambo ya kidesturi.”
Kwa wazi, mwaka wa 1914 ulikuwa muhimu katika historia. Broshua yenye kurasa 32 Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai? Wewe Waweza Kulipataje? huzungumzia jambo lilo hilo. Unaweza kupokea broshua hiyo kwa kujaza na kupeleka kuponi iliyopo hapa ukitumia anwani iliyoonyeshwa, au anwani ihusuyo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Nipelekeeni broshua Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai? Wewe Waweza Kulipataje?
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.