Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi Wakristo wa Mapema Walivyoandika Maandishi Matakatifu
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Septemba 1
    • Inaonekana kwamba mabamba yenye nta yalipatikana kwa urahisi na yangetumiwa kuandika habari. Mfano mmoja wa jambo hilo unaonekana katika sura ya kwanza ya Luka. Zekaria, ambaye alikuwa amepoteza uwezo wake wa kuzungumza kwa muda, aliulizwa alitaka mwana wake aitwe jina gani. Mstari wa 63 unasema hivi: “Akaomba bamba [huenda kwa kutumia ishara] na kuandika: ‘Yohana ndilo jina lake.’” Kamusi za Biblia zinaeleza kwamba neno “bamba” huenda lilirejelea ubao wa kuandika uliofunikwa kwa nta. Huenda mtu fulani hapo alikuwa na ubao ambao Zekaria angeweza kuandikia.

      Kuna mfano mwingine unaoonyesha kwamba vibao vya kuandika na matumizi yake yalijulikana wakati huo. Katika kitabu cha Matendo, tunasoma kwamba Petro alipokuwa akizungumza na umati kwenye eneo la hekalu aliwahimiza hivi: “Tubuni . . . dhambi zenu zipate kufutwa.” (Matendo 3:11, 19) Maneno “zipate kufutwa” yanatokana na kitenzi cha Kigiriki kinachomaanisha “futa.” Kamusi moja (The New International Dictionary of New Testament Theology) inaeleza hivi: “Inawezekana kwamba wazo linalotolewa na kitenzi hicho hapo na kwingineko ni lile la kulainisha sehemu ya juu ya ubao wa kuandika wenye nta ili utumike tena.”

  • Jinsi Wakristo wa Mapema Walivyoandika Maandishi Matakatifu
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Septemba 1
    • [Picha katika ukurasa wa 13]

      “Akaomba bamba na kuandika: ‘Yohana ndilo jina lake’”

      [Picha katika ukurasa wa 13]

      Bamba lililo na nta likiwa na vifaa vya kuandikia vya karne ya kwanza au ya pili W.K.

      [Hisani]

      © British Museum/Art Resource, NY

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki