-
Ripoti ya Ulimwenguni Pote2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Rwanda
Wakati fulani uliopita, wapita-njia waliokota barabarani kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Walikipeleka kwa mzee wa kanisa lao la Kiprotestanti. Mzee huyo alikisoma kitabu hicho na kikampendeza sana. Aliwatafuta Mashahidi na akaanza kujifunza Biblia pamoja nao. Ujuzi wake kuhusu kweli ya Biblia uliongezeka, kwa hiyo akaacha kanisa lake na kubatizwa. Wakati huohuo, aliwahubiria kwa bidii waumini wengine katika kanisa lake la zamani kuhusu kweli. Waumini 25 waliacha kanisa hilo na kuwa Mashahidi wa Yehova. Mtu aliyechukua mahali pake kama mzee wa kanisa alianza kujifunza Biblia na Mashahidi, naye pia akaacha kanisa hilo. Sasa anahudhuria mikutano ya Kikristo na anataka kuwa mhubiri. Mke wake alibatizwa kwenye kusanyiko la pekee lililofanywa hivi majuzi. Ajabu ni kwamba watu hao wote wamejifunza kweli kwa sababu ya kitabu kilichookotwa barabarani!
-
-
Ripoti ya Ulimwenguni Pote2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 48]
Baadhi ya watu waliokuwa waumini wa lile kanisa
-