Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ninaweza kuepukaje ngono kati ya watu wa jinsia moja?
    Amkeni!—2007 | Februari
    • Ukiwa kijana, huenda ukawa unakabili hisia mbalimbali. Vipi ikiwa unavutiwa kingono na mtu wa jinsia yako? Je, hilo linaonyesha wazi kwamba utakuwa shoga? Hapana. Kumbuka, uko katika “upeo wa ujana,” kipindi ambacho unasisimuka kingono bila kutaka. (1 Wakorintho 7:36) Kwa muda fulani huenda ukavutiwa kingono na mtu wa jinsia yako. Lakini kuwa na hisia hizo hakumaanishi kwamba utakuwa shoga. Takwimu zinaonyesha kwamba kwa kawaida hisia hizo hutoweka baada ya muda. Lakini huenda bado unajiuliza, ‘Chanzo cha hisia hizo ni nini?’

      Watu wengine wanasema kwamba ushoga upo kwenye chembe za urithi. Wengine wanasema kwamba mtu hujifunza zoea hilo. Si kusudi la makala hii kujadili ikiwa zoea hilo ni la kurithiwa au ni la kujifunza. Kwa wazi, kusema kwamba ushoga unasababishwa na jambo fulani hususa haingekuwa kweli. Inaonekana kwamba kama ilivyo kwa mazoea mengine, ni vigumu kufahamu chanzo cha zoea hilo.

      Hata chanzo kiwe nini, jambo muhimu ni kutambua kwamba Biblia inashutumu ngono kati ya watu wa jinsia moja. Hivyo, mtu anayevutiwa kingono na mtu wa jinsia yake anaweza kushinda tatizo hilo kwa kutotenda kulingana na tamaa hizo. Kwa mfano: Mtu anaweza kuwa na “mwelekeo wa ghadhabu.” (Methali 29:22) Huenda zamani alizoea kulipuka kwa hasira. Lakini baada ya kujifunza Biblia, anaona uhitaji wa kujizuia. Je, hilo linamaanisha kwamba hatawahi tena kupandwa na hasira? Hapana. Hata hivyo, kwa kuwa anajua yale ambayo Biblia inasema kuhusu hasira isiyodhibitiwa, hatendi kulingana na hisia zake. Hivyo ndivyo ilivyo kwa mtu anayevutiwa na mtu wa jinsia yake, lakini sasa amejifunza maoni ya Biblia kuhusu ngono kati ya watu wa jinsia moja. Mara kwa mara, anaweza kurudiwa na tamaa hizo zisizofaa. Hata hivyo, kwa kutii shauri la Biblia, mtu anaweza kukataa kutenda kulingana na tamaa hizo.

      Ni kweli kwamba huenda tamaa ya kufanya ngono na mtu wa jinsia yako ikawa imekita mizizi. Uwe na hakika, kwamba hata tamaa hiyo iwe imekita mizizi namna gani, unaweza kuishinda. (1 Wakorintho 9:27; Waefeso 4:22-24) Kwa vyovyote vile, wewe ndiye utakayeamua jinsi utakavyoishi. (Mathayo 7:13, 14; Waroma 12:1, 2) Na licha ya madai ya wengi, unaweza kujifunza kuthibiti tamaa zako na hata kuamua kutotenda kulingana na tamaa hizo—au hata kujifunza kuzidhibiti.

  • Ninaweza kuepukaje ngono kati ya watu wa jinsia moja?
    Amkeni!—2007 | Februari
    • Vijana Huuliza . . .

      Ninaweza kuepukaje ngono kati ya watu wa jinsia moja?

      “Nilipokuwa na umri wa miaka 12, nilivutiwa na msichana mwenzangu shuleni. Nilichanganyikiwa na kuhofia kwamba huenda nikawa ninavutiwa kingono na watu wa jinsia yangu.”—Anna.a

      “Nilipokuwa kijana, nilipambana na hisia za kuvutiwa kingono na wanaume wengine. Moyoni, nilijua kwamba hisia hizo si za kawaida.”—Olef.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki