Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ninaweza Kuwa Rafiki ya Mungu Jinsi Gani?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
    • Faida ya Kujifunza

      Marafiki huwasiliana—kila mmoja husikiliza na kuzungumza. Ndivyo pia na urafiki pamoja na Mungu. Tunaposoma na kujifunza Biblia, tunamsikiliza Mungu.—Zaburi 1:2, 3.

      Ni kweli kwamba huenda kiasili hupendi kusoma. Vijana wengi hupenda kutazama televisheni, kucheza, au kuwa tu na marafiki. Lakini ikiwa unataka kuwa rafiki ya Mungu, hakuna njia ya mkato. Lazima umsikilize kwa kujifunza Neno lake.

      Hata hivyo, usiwe na wasiwasi. Si lazima kujifunza kuwe jambo lenye kuchosha. Unaweza kujifunza kufurahia kufanya hivyo—hata ikiwa kiasili hupendi kusoma. Jambo la kwanza unalohitaji kufanya ni kutenga wakati wa kujifunza Biblia. “Mimi nina ratiba,” anasema msichana mmoja anayeitwa Lais. “Mimi husoma sura moja ya Biblia kila asubuhi ninapoamka.” Maria, mwenye umri wa miaka 15, ana ratiba tofauti. “Mimi husoma sehemu fulani ya Biblia kila siku kabla ya kwenda kulala,” anasema.

      Ili kuanza programu yako mwenyewe ya kujifunza, tazama sanduku lililo katika ukurasa wa 292. Kisha, katika nafasi iliyo hapa chini, andika wakati ambapo unaweza kutumia dakika 30 hivi ukijifunza Neno la Mungu.

      ․․․․․

      Kupanga wakati ni hatua ya kwanza tu. Ukishaanza kujifunza, huenda ukaona kwamba nyakati nyingine si rahisi kusoma Biblia. Huenda ukakubaliana na Jezreel, mwenye umri wa miaka 11, aliyesema hivi waziwazi: “Sehemu fulani za Biblia ni ngumu na si zenye kusisimua sana.” Ikiwa unahisi hivyo, usikate tamaa. Sikuzote ona wakati wa kujifunza kuwa wakati wa kumsikiliza Yehova Mungu, rafiki yako. Mwishowe, kujifunza Biblia kutakuwa jambo lenye kusisimua na lenye faida kwako ikitegemea jitihada zako!

  • Ninaweza Kuwa Rafiki ya Mungu Jinsi Gani?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 292]

      Ichanganue Biblia

      1. Chagua simulizi fulani katika Biblia ambalo ungependa kusoma. Sali upate hekima ya kuelewa habari hiyo.

      2. Soma simulizi hilo kwa uangalifu. Usiwe na haraka. Unaposoma, piga picha akilini. Jiwazie ukiwa katika hali unayosoma: Jaribu kuona kinachoendelea, kusikia sauti mbalimbali, vuta pumzi na kunusa harufu mbalimbali, onja ladha ya chakula, na kadhalika. Fanya simulizi hilo liwe halisi akilini mwako!

      3. Fikiria habari ambayo umesoma. Jiulize maswali kama vile:

      ● Kwa nini Yehova alitia ndani simulizi hilo katika Neno lake?

      ● Ni nani wanaostahili kuigwa, na ni nani walio vielelezo vya kuonya?

      ● Ni jambo gani la maana ninaloweza kujifunza kutokana na usomaji huo?

      ● Simulizi hilo linanifundisha nini kuhusu Yehova na jinsi anavyofanya mambo?

      4. Toa sala fupi kwa Yehova. Mwambie mambo ambayo umejifunza kutokana na funzo lako la Biblia na jinsi unavyopanga kutumia habari hiyo maishani mwako. Mshukuru Yehova sikuzote kwa zawadi ambayo amekupa—Neno lake, Biblia Takatifu!

      [Picha]

      “Neno lako ni taa ya mguu wangu, na nuru kwa barabara yangu.”—Zaburi 119:105.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki