-
Unakadiriaje Mafanikio?Mnara wa Mlinzi—2000 | Novemba 1
-
-
Wakati Utamaduni na Dhamiri Zinapopingana
Robert alilelewa akiwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Ujanani, mwenendo wake na mashirika yake yakawa mabaya. Mama yake akaanza kuwa na wasiwasi kumhusu. Kwa hiyo, akamwomba painia mmoja, mhudumu wa wakati wote wa Mashahidi wa Yehova, amtie moyo. Robert aeleza yaliyotukia baadaye.
“Nilithamini sana jinsi ndugu huyo painia alivyonijali. Kielelezo chake bora kilinifanya nitake kuufanya upainia uwe kazi-maisha mara tu nilipomaliza shule. Ndipo mama akawa na wasiwasi tena—lakini kwa sababu tofauti. Katika utamaduni wetu ni sawa kwa msichana kuanza upainia mara tu amalizapo shule, lakini mvulana hutazamiwa afanye kazi na kupata fedha kwanza kisha anaweza kufikiria kupainia.
“Nilijifunza kazi fulani ya ufundi na kuanzisha biashara yangu. Upesi nilijiingiza sana katika biashara hiyo na nilikuwa ninahudhuria mikutano na kuhubiri kama desturi tu. Dhamiri yangu ilinisumbua—nilijua ningeweza kumtumikia Yehova kikamili zaidi. Hata hivyo, nilijikakamua kwelikweli kutofanya yale ambayo wengine walitazamia nifanye, na ninafurahi nilifanya hivyo. Sasa nimeoa, na mimi na mke wangu tumekuwa mapainia kwa muda wa miaka miwili iliyopita. Hivi karibuni, niliwekwa kuwa mtumishi wa huduma kutanikoni. Ninaweza kusema kwa unyofu kwamba sasa ninahisi nimeridhika kikweli kwa kumtumikia Yehova kwa moyo wangu wote, kadiri niwezavyo.”
Mara nyingi gazeti hili limewatia moyo vijana wajifunze kazi fulani au wasitawishe stadi mbalimbali zenye manufaa—wakiwa bado shuleni iwapo yawezekana. Kwa kusudi gani? Ili wawe matajiri? La. Sababu kuu ni ili waweze kujitegemeza ifaavyo wakiwa watu wazima na kumtumikia Yehova kwa kadiri wawezavyo, hasa katika huduma ya wakati wote. Hata hivyo, mara kwa mara imetokea kwamba vijana wanaume na wanawake hujishughulisha sana na kazi-maisha ya ulimwengu hivi kwamba huduma inakuwa si muhimu sana. Baadhi yao hawafikirii utumishi wa wakati wote hata kidogo. Kwa nini?
Maelezo ya Robert yanafafanua jambo hili. Baada ya kujifunza kazi, Robert alianzisha biashara. Muda si muda akawa anafanya kazi yenye kuchosha isiyokuwa na matokeo. Alikusudia kupata fedha za kutosha. Lakini je, kuna yeyote ndani au nje ya kutaniko la Kikristo anayeweza kupata fedha za kutosha? Wakristo wanapaswa kujitahidi kuwa wenye kuwajibika kifedha, wakijitahidi sana kutimiza matakwa yao ya kifedha; lakini wanapaswa pia kutambua kwamba katika nyakati hizi zisizo na uhakika, ni wachache ambao hufikia hatua wanapoweza kwa kweli kuona kwamba wana fedha za kutosha. Hiyo ndiyo sababu ahadi ya Yesu kwenye Mathayo 6:33 inawafariji sana Wakristo.
Robert anafurahi kwamba aliamua kufuata tamaa za moyo wake badala ya kufanya vile utamaduni wa kwao ulivyotaka afanye. Leo, yeye anafurahia kazi-maisha ya utumishi wa wakati wote. Naam, huduma ya wakati wote ni kazi-maisha yenye kuheshimika. Robert ana amani kwa sababu anamtumikia Yehova, kama asemavyo, ‘kwa uwezo wake wote.’
-
-
Unakadiriaje Mafanikio?Mnara wa Mlinzi—2000 | Novemba 1
-
-
Vivyo hivyo leo, wengine wametumia vipawa vyao na hata elimu yao ili kuendeleza masilahi ya Ufalme. Kwa mfano, Amy ana digrii ya chuo kikuu ya mambo ya biashara na nyingine ya uanasheria. Wakati mmoja alikuwa na kazi yenye mapato makubwa, lakini leo anatumikia akiwa mjitoleaji asiyelipwa mshahara katika mojawapo ya ofisi za tawi za Watch Tower Society. Amy anaeleza hivi kuhusu maisha yake ya sasa: “Ninaamini kwamba nimefanya uamuzi ufaao kabisa maishani. . . . Sitaki hata kufanya kazi wanazofanya wale niliosoma nao chuoni. Ninajivunia kazi niliyochagua kufanya. Nina kila kitu ninachohitaji na ninachotaka—maisha yenye kuridhisha na yenye furaha na kazi-maisha yenye kuridhisha pia.”
-