Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo (Kinshasa)
    2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
    • Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Wamletea Yehova Sifa

      Katika miaka ya karibuni, Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova limefanya jitihada ya pekee ya kusaidia kujenga Majumba ya Ufalme katika nchi maskini. Ndugu Wakongomani walifurahia sana mpango huo kwa sababu kulikuwa na uhitaji mkubwa sana wa Majumba ya Ufalme. Kwa mfano, jiji la Kinshasa lilikuwa na makutaniko 298, lakini idadi ya majumba yanayofaa haikuzidi 20. Mamia ya majumba yalihitajiwa nchini kote. Katika Aprili 1999, mpango wa ujenzi wa Majumba ya Ufalme ulianza huko Kinshasa. Baadaye, ujenzi ulianza kwenye majimbo mengine ya Kongo. Kufikia mwanzoni mwa mwaka wa 2003, Majumba ya Ufalme yapatayo 175 yalikuwa yamejengwa katika nchi mbili za Kongo.

      Mtu mmoja aliyefahamu kweli tangu miaka ya 1950 alifurahi sana kuona Jumba la Ufalme likijengwa mbele ya nyumba yake. Alisema: “Sikupendezwa na kazi ya Mashahidi. Sasa naona matokeo ya jitihada zao. Walijenga Jumba la Ufalme karibu na nyumba ya kaka yangu, na sasa kuna Jumba la Ufalme mbele ya nyumba yangu. Ni kana kwamba Mashahidi wananifuata popote niendapo!” Mtu huyo alikubali mwaliko wa kuhudhuria Ukumbusho wa kifo cha Kristo na kuwekwa wakfu kwa Jumba hilo jipya la Ufalme. Sasa anahudhuria mikutano kwa ukawaida.

      Makutaniko matatu huko Matete yalifanya mikutano kwenye jengo lililochakaa, ambalo walinunua mwaka wa 1994. Akina ndugu hawakuwa na pesa za kurekebisha jengo hilo, basi lilibaki hivyo kwa miaka sita. Kulikuwa na kanisa kubwa ng’ambo ya barabara. Kanisa hilo lilipojengwa, kasisi alisema kwamba Mashahidi wa Yehova watahama karibuni. Majirani waliwadhihaki akina ndugu kwa sababu hawakuwa na mahali pazuri pa mikutano. Hata kutaniko lilipoanza kutengeneza matofali ya Jumba jipya la Ufalme, majirani fulani waliendelea kuwadhihaki. Walishangaa sana walipoona matokeo! Sasa wanasema kwamba jengo la Mashahidi wa Yehova ndilo maridadi zaidi katika eneo hilo. Jirani mmoja ambaye hakutaka kamwe kuongea na Mashahidi hapo awali alivutiwa na kazi iliyofanywa na akina ndugu. Alikuja mahali pa ujenzi akaahidi kwamba atawasikiliza Mashahidi watakapomtembelea.

      Katika sehemu moja ambapo ujenzi ulikuwa ukiendelea, mwanamke fulani alimfikia dada aliyekuwa akiwapikia wafanyakazi. Mwanamke huyo akamuuliza: “Je, mnajenga kanisa?”

      “Tunajenga Jumba letu la Ufalme,” dada akamjibu.

      Mwanamke huyo akasema: “Jengo hili litakuwa kama ninyi mlivyo. Ninyi huwa safi na nadhifu sikuzote. Kanisa lenu litakuwa kama ninyi!”

  • Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo (Kinshasa)
    2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
    • [Picha katika ukurasa wa 252, 253]

      (1) Majengo ya Betheli ya Kinshasa

      (2-4) Majumba mapya ya Ufalme

      (5) Ndugu asaidia katika ujenzi wa Jumba la Ufalme

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki