-
Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo (Kinshasa)2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
-
-
Kwa miaka mingi akina ndugu hawakuweza kupanga makusanyiko makubwa ya wilaya. Sasa walikuwa huru kufanya hivyo. Mnamo mwaka wa 1980, Makusanyiko matano ya Wilaya ya “Upendo wa Kimungu” yalifanywa nchini kote. Baadhi ya ndugu walisafiri mbali sana. Familia nyingi zilitembea umbali wa zaidi ya kilometa 400 ili kuhudhuria. Mapainia wawili wa pekee kutoka eneo la mbali sana walisafiri kwa majuma mawili zaidi ya kilometa 700 kwa baiskeli zao, kupitia kwenye mchanga mwingi na msitu mkubwa wa mvua. Ndugu fulani hata walitoka Kongo (Brazzaville), Burundi, na Rwanda.
Katika miaka iliyofuata, kulikuwa na uhitaji wa kupanga makusanyiko ya wilaya katika sehemu nyingi zaidi. Ni kweli kwamba ndugu walikuwa na uhuru wa kuabudu, lakini matatizo ya kiuchumi yalizidi kuongezeka. Wengi walishindwa kupata hata mahitaji ya lazima. Bei zilipanda, lakini mishahara haikuongezwa. Nauli ya magari ilikuwa juu sana hivi kwamba ndugu wengi hawakuweza kusafiri mbali. Kwa hiyo, ofisi ya tawi ilionyesha upendo kwa kufanya makusanyiko karibu na maeneo ambayo ndugu wengi waliishi.
Kwa kweli si rahisi kusafiri kwenye barabara za Kongo. Ni kawaida kupata miti iliyoanguka barabarani, madaraja yaliyoharibika, mchanga mwingi, na mashimo yenye matope. Wawakilishi wa ofisi ya tawi na wake zao hujidhabihu sana wanapotumikia kwenye makusanyiko. Lakini, ndugu na dada waaminifu ambao ni wenyeji hujidhabihu hata zaidi kwa sababu mara nyingi wao hulazimika kutembea kwa siku nyingi na kulala vichakani. Bado ndugu wengi hutembea umbali wa kati ya kilometa 50 na 150 ili kuhudhuria makusanyiko ya wilaya.
-
-
Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo (Kinshasa)2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
-
-
[Picha katika ukurasa wa 221]
Kusanyiko la Wilaya la “Upendo wa Kimungu” huko Kinshasa, mwaka wa 1980, lilikuwa kusanyiko kubwa la kwanza kufanywa huko baada ya miaka minane
-
-
Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo (Kinshasa)2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
-
-
[Picha katika ukurasa wa 223]
Wengi hutembea kwa siku nyingi wakiwa wamebeba vyakula na mizigo mingine ili kuhudhuria makusanyiko
-