-
Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo (Kinshasa)2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
-
-
Tangu Januari [12], 1949, kazi ya Watch Tower Society imepigwa marufuku katika Kongo ya Ubelgiji na mashahidi wa kweli wa Yehova wameteswa kwa sababu ya ripoti hizo za uwongo. Barua za malalamiko zimeandikwa na kupelekwa kwa waziri wa koloni, na uthibitisho wa kutosha umetolewa kuonyesha kwamba Mashahidi wa Yehova na Watch Tower Society hawana uhusiano wowote na kikundi cha mapinduzi cha “Kitawala,” lakini malalamiko hayo hayajajibiwa.
Njia zifuatazo zimetumiwa ili kujaribu kukomesha kabisa kazi ya ‘kuhubiri Neno’ katika Kongo ya Ubelgiji: kueneza habari za uwongo, kuwatesa ndugu, kuwatoza faini, kuwapiga, kuwafunga gerezani, na kuwafukuza nchini.
1952: Kama huko Ulaya Mashariki, kuna “pazia la chuma” pia katika Afrika ya Kati! Kwa maoni ya mashahidi wa Yehova, pazia hilo limezingira Kongo ya Ubelgiji. Kazi ya kuhubiri ingali imepigwa marufuku katika nchi hiyo yenye Wakatoliki wengi.
-
-
Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo (Kinshasa)2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
-
-
1949: Sheria yatungwa kuthibitisha kwamba Mashahidi wa Yehova wamepigwa marufuku.
-