-
Zambia2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Utumishi wa wakati wote ulifanya Bernard Musinga, mke wake Pauline, na watoto wao wachanga wahamie nchi kama vile Uganda, Kenya, na Ethiopia. Bernard anasema hivi kuhusu ziara yake huko Shelisheli: “Katika 1976, niliombwa kutembelea kikundi fulani katika kisiwa maridadi cha Praslin. Wakaaji wa huko walikuwa wafuasi thabiti wa Kanisa Katoliki, na tayari kulikuwa na matatizo. Kwa mfano, mvulana wa mhubiri fulani alikuwa amekataa kuandika alama ya kujumlisha katika somo la hesabu, na kueleza: ‘Huo ni msalaba, nami siamini msalaba.’ Baada ya kisa hicho, viongozi wa dini walitushutumu wakisema: ‘Mashahidi wa Yehova hawawaruhusu watoto wao wajifunze hesabu.’ Kwenye mkutano pamoja na waziri wa elimu tulifafanua kwa heshima imani yetu na kusuluhisha tatizo hilo. Urafiki wetu pamoja na waziri huyo ulimfanya awasaidie wamishonari kuingia kisiwani humo.”
-
-
Zambia2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha]
Pauline na Bernard Musinga
-