-
Zambia2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Mnamo Machi 1936, katibu wa nchi alikubali depo ya vichapo ifunguliwe huko Lusaka na Llewelyn Phillips awe mwakilishi.
-
-
Zambia2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Katika miaka iliyofuata, Ndugu Phillips alifanya kazi kwa bidii pamoja na ndugu wengine ili kuwasaidia na kuwaimarisha wale wenye mioyo minyoofu na kuwaondosha wale walioendeleza mazoea yasiyopatana na maandiko. Mapainia walifundishwa kuhusu mafundisho ya Biblia, maadili, na utaratibu wa tengenezo, kisha wakatumwa kusaidia vikundi na makutaniko.
-
-
Zambia2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Llewelyn Phillips alimwandikia gavana akilalamika kuhusu vichapo vilivyokuwa vimepigwa marufuku. Ndugu Phillips, ambaye alikuwa amefungwa mapema mwaka huohuo kwa sababu ya kutojiandikisha jeshini, alifungwa miezi mingine sita. Mfanyakazi wa kujitolea aliyefanya kazi katika depo ya vichapo huko Lusaka alisema: “Mara kwa mara maofisa wa Idara ya Upelelezi wa Jinai walikuja, na mara nyingi Ndugu Phillips aliitwa kwenye kituo cha polisi.” Hata hivyo, Ndugu Phillips aliendelea kusaidia makutaniko yawe na utaratibu na bidii. Ndugu wenye uwezo walipopatikana, walizoezwa na kutumwa wakiwa wahudumu, au waangalizi, wanaosafiri. Jitihada zao zilichangia ongezeko kwa kuwa katika 1943 kulikuwa na kilele cha wahubiri 3,409.
-
-
Zambia2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 170]
Llewelyn Phillips
-