-
Zambia2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Geoffrey Wheeler anasema: “Majuma matatu tu baada kuwekwa kuwa mwangalizi wa wilaya tulikabili tatizo. Tulikuwa mahali ambapo tungefanyia kusanyiko na tulikuwa tayari kwa ajili ya programu ya mwisho wa juma. Nilikuwa nimepewa stovu fulani mbovu. Kulikuwa na joto na upepo, na nilipoiwasha, moto ulienea ghafula. Muda si muda, moto huo ukawa mkubwa sana. Gurudumu moja la gari letu lilishika moto na upesi moto ukaenea garini mwote.”
Ilikuwa hasara kubwa kwao kupoteza gari, lakini kulikuwa na matatizo mengine pia. Geoffrey anasema: “Nguo zetu zilikuwa kwenye sanduku la chuma garini. Hazikuteketea lakini ziliharibika. Ndugu walienda upande wa gari ambao haukuwa umeshika moto na kuondoa kitanda chetu, shati, na taipureta yangu. Tuliwashukuru sana kwa kuchukua hatua haraka.” Kwa kuwa vitu vyao viliharibika garini, nao walitazamia kurudi mjini baada ya miezi miwili, walifanyaje? Geoffrey anasema: “Ndugu mmoja alinipa tai na nikatoa hotuba ya watu wote nikiwa nimevalia viatu vikubwa. Tulifaulu kuendelea na kazi yetu na ndugu wakajitahidi sana kumfariji mwangalizi wao wa wilaya ambaye hakuwa na ujuzi.”
-
-
Zambia2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Mashambani watu hupewa zawadi mbalimbali. Geoffrey Wheeler anasema: “Pindi moja tulipewa kuku na akina ndugu. Kabla usiku haujaingia, tulimweka chooni alale hapo. Lakini kiumbe huyo mpumbavu aliruka na kuingia ndani ya shimo la choo. Tulimwokoa kwa kutumia jembe. Kisha mke wangu akamwosha kwa maji ya moto yenye sabuni na dawa nyingi. Tulimpika mwishoni mwa juma naye alikuwa mtamu wee!”
-