-
Zambia2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Ilikuwa vigumu kuwatambua wale ambao kwa kweli walikuwa na nia ya kumtumikia Mungu. Katika 1924, Thomas Walder na George Phillips, kutoka Uingereza, waliwasili kwenye ofisi ya Wanafunzi wa Biblia huko Cape Town, Afrika Kusini. Ndugu Walder, aliyekuwa na miaka 30 na kitu, alisafiri katika eneo lote la Rodeshia ili kuchunguza ni nani waliohusianishwa na jina Watch Tower.
-
-
Zambia2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Ijapokuwa watu hawakukatazwa wasijifunze Biblia wala wasikutanike kwa ajili ya ibada, Ndugu Walder aliviandikia vikundi vya watu waliopendezwa na kuwahimiza wafuate mpango huo hadi wakati ambapo ingewezekana kuwa na mwakilishi wa kudumu wa Wanafunzi wa Biblia nchini humo.
-