Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zambia
    2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Ashikwa na Woga Jukwaani!

      Bado drama za Biblia ni sehemu inayopendwa sana ya programu za makusanyiko. Kila mhusika huchukua kwa uzito wajibu wake wa kuonyesha hisia za mtu anayeigizwa, na Wazambia wengi huigiza sehemu zao kwa juhudi. Frank Lewis, ambaye alikuwa mmishonari na sasa ni Mwanabetheli huko Marekani, anasema: “Zamani hatukurekodi drama katika kaseti. Ndugu walioigiza sehemu mbalimbali walihitaji kukariri maneno yao. Nakumbuka wakati tulipofanya drama yetu ya kwanza iliyomhusu Yosefu kwenye kusanyiko moja katika Mkoa wa Kaskazini. Kwa kuwa barua zilichelewa na ndugu hawakuwa wamepata hati zao, ilitubidi kufanya mazoezi hadi usiku sana ili ndugu waweze kukariri sehemu zao. Drama ilipokuwa ikifanywa, tulifikia sehemu ambayo mke wa Potifa anamweleza mume wake kwamba Yosefu alitaka kulala naye kinguvu. Ndipo ndugu aliyekuwa akiigiza sehemu ya Potifa aliposhikwa na woga na kuondoka jukwaani. Nilikuwa nyuma ya jukwaa nikiwakumbusha akina ndugu maneno yao nilipomwona akiondoka jukwaani. Nilimkumbusha haraka maneno yake ya kwanza na kumsukuma tena jukwaani. Kisha akasema vizuri maneno yake yenye dharau kumhusu mwanamume huyo aliyeshtakiwa kwa kutaka kulala kinguvu na mke wake! Ijapokuwa mambo yalikuwa karibu kuharibika kusanyikoni, kila mara ninaposoma masimulizi hayo ya Biblia mimi husema: ‘Huenda ilikuwa hivyo. Labda Potifa aliondoka chumbani kwa hasira, na baada ya kutulia, akarudi ili kumshutumu Yosefu!’”

      Mnamo 1978, ile sheria ambayo ilitumiwa kwa miaka minne kuzuia makusanyiko makubwa yasifanywe, iliondolewa. Hata hivyo, ilikuwa vigumu kufanya kusanyiko la “Imani Yenye Ushindi” mwaka huo. Ndugu mmoja ambaye zamani alikuwa mwangalizi anayesafiri anasema: “Katika kusanyiko hilo tulifanya drama zote zilizopaswa kufanywa katika miaka iliyotangulia, wakati ambapo tulilazimika kukutanika kwenye Majumba ya Ufalme. Lilikuwa kusanyiko la siku tano, na tulifanya drama tano, yaani, drama moja kila siku. Tulitazama drama zote tulizokuwa tumezikosa! Wote walizifurahia lakini mwakilishi wa Betheli alikuwa na kazi ngumu ya kukagua drama hizo zote. Ilikuwa kazi nyingi sana!”

  • Zambia
    2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 215]

      Kushoto: Drama ya Biblia, 1991

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki