-
Zambia2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Katika 1957, William Lamp Chisenga aliombwa awe painia wa pekee katika milima inayozunguka Mbeya, Tanzania. “Mimi na mke wangu, Mary, na wana wetu wawili tulifika huko katika mwezi wa Novemba, na tukakaa usiku kucha katika kituo cha basi kwa kuwa hoteli zilikuwa zimejaa. Ijapokuwa kulikuwa na baridi na mvua usiku, tulitarajia kuona jinsi ambavyo Yehova angeelekeza mambo. Asubuhi iliyofuata, niliiacha familia yangu kituoni na nikaenda kutafuta nyumba. Sikujua niende wapi lakini nilibeba nakala za Mnara wa Mlinzi. Nilipofika kwenye posta nikiwa tayari nimegawa magazeti kadhaa, nilikutana na mwanamume fulani anayeitwa Johnson. Mwanamume huyo aliniuliza: ‘Unatoka wapi, na unaenda wapi?’ Nikamwambia nimekuja kuhubiri habari njema. Alipojua kuwa mimi ni Shahidi wa Yehova, alisema kwamba anatoka Lundazi, katika Mkoa wa Mashariki wa Zambia, na kwamba yeye ni Shahidi aliyekuwa ameacha kutenda. Tulifanya mipango ya kuipeleka familia yangu na mizigo yetu nyumbani kwake. Baada ya muda, Johnson na mke wake waliimarika tena kiroho, nao wakatusaidia kujifunza Kiswahili. Hatimaye, alirudi Zambia na akawa mhubiri mwenye bidii wa habari njema. Jambo hilo lilinifundisha kutopuuza uwezo wa Yehova wa kutusaidia na vilevile kutopuuza nafasi za kuwasaidia wengine.”
-
-
Zambia2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha]
William Lamp Chisenga
-