-
Ujenzi wa Kiroho Katika “Nyumba ya Mawe”Mnara wa Mlinzi—2007 | Februari 15
-
-
Kujenga Nyumba za Ibada
Mtungaji wa mashairi aliyeongozwa na roho aliandika hivi: “Ee Mungu, . . . nafsi yangu ina kiu kwa ajili yako. . . . Katika nchi iliyokauka na kuchoka, ambapo hakuna maji.” (Zaburi 63:1) Maneno hayo yamethibitika kuwa ya kweli kwa watu wengi nchini Zimbabwe! Kimwili wanavumilia ukame, lakini kiroho wana kiu kwa ajili ya Mungu na wema wake. Unaweza kuona hilo kupitia matokeo ya huduma ya Kikristo ya Mashahidi wa Yehova. Zimbabwe ilipopata uhuru mwaka wa 1980, Mashahidi 10,000 hivi walikuwa wakitumika katika makutaniko 476. Sasa, miaka 27 baadaye, idadi ya Mashahidi wanaotenda ni mara tatu zaidi na idadi ya makutaniko ni karibu mara mbili.
Ni makutaniko machache yaliyokuwa na mahali pa ibada. Mnamo Januari (Mwezi wa 1) 2001, ni makutaniko 98 tu kati ya makutaniko 800 nchini Zimbabwe yalikuwa na nyumba ya ibada, yaani, Jumba la Ufalme la kufanyia mikutano. Makutaniko mengi yalifanyia mikutano chini ya miti au katika vibanda vya miti, vyenye kuta za udongo na paa za nyasi.
Kwa sababu ya michango ya ukarimu na kazi ya bidii ya kujitolea ya ndugu zao Wakristo wa ulimwenguni pote, Mashahidi nchini Zimbabwe wameanza programu ambayo inayawezesha makutaniko mengi zaidi kupata Majumba ya Ufalme yanayofaa na yenye kuheshimika. Mashahidi wengi kutoka nchi za ng’ambo ambao wana ustadi wa ujenzi walifanya mipango ya kwenda Zimbabwe na kufanya kazi pamoja na wafanyakazi wa kujitolea wa nchi hiyo. Shahidi mmoja wa Zimbabwe aliandika hivi: “Tunawashukuru kutoka moyoni ndugu na dada wote wa nchi nyingi ambao wamekuja Zimbabwe ili kutusaidia kujenga Majumba maridadi ya Ufalme. Na pia tunawashukuru wengine wote kwa sababu ya michango mnayotoa kwa ajili ya Hazina ya Majumba ya Ufalme ambayo inafanikisha kazi hii.”
Katika sehemu ya mashariki ya nchi hiyo, akina ndugu walikutanika chini ya mti mkubwa wa mbuyu kwa muda wa miaka 50. Wazee Wakristo walipoambiwa kwamba nyumba halisi ya ibada ingejengwa, mzee mmoja kati yao alitokwa na machozi. Katika kutaniko moja la karibu, mzee mmoja mwenye umri wa miaka 91 alisema hivi: “Nimekuwa nikimlilia Yehova kwa miaka mingi sana ili jambo kama hili litukie!”
Watu wengi wameeleza jinsi majengo hayo yenye kuvutia yanavyojengwa kwa haraka. Mtu mmoja alisema hivi: “Ninyi watu mnajenga wakati wa mchana, lakini lazima Mungu awe anajenga usiku!” Umoja na furaha ya wafanyakazi inaonekana pia. Kufikia sasa, Majumba mapya ya Ufalme zaidi ya 350 yamekamilishwa nchini kote. Hivyo, makutaniko 534 yanakutana katika Majumba ya Ufalme yaliyo imara ambayo yamejengwa kwa matofali.
-
-
Ujenzi wa Kiroho Katika “Nyumba ya Mawe”Mnara wa Mlinzi—2007 | Februari 15
-
-
[Picha katika ukurasa wa 12]
Jumba jipya la Ufalme, Kutaniko la Concession
[Picha katika ukurasa wa 12]
Washiriki wa Kutaniko la Lyndale nje ya Jumba lao Jipya la Ufalme
-