-
Yehova Anajua Jinsi ya Kuwakomboa Watu WakeMnara wa Mlinzi—2012 | Aprili 15
-
-
KUPONYOKA UHARIBIFU WA YERUSALEMU
13. Yesu alitoa maagizo gani, na huenda wafuasi wake walijiuliza nini?
13 Yehova anajua ni namna gani hasa matukio yatakavyoanza ili kutimiza kusudi lake. Umuhimu wa jambo hilo unakaziwa katika mfano wa tatu ambao tutachunguza: kuzingirwa kwa Yerusalemu katika karne ya kwanza. Kupitia Mwana wake, Yehova aliandaa maagizo ya jinsi ya kuokoka kwa ajili ya Wakristo waliokuwa wakiishi Yerusalemu na Yudea kabla ya uharibifu wa jiji hilo katika mwaka wa 70 W.K. Yesu alisema hivi: “Mtakapoona lile chukizo linalosababisha ukiwa, kama vile lilivyosemwa kupitia nabii Danieli, likiwa limesimama katika mahali patakatifu, . . . ndipo wale walio katika Yudea waanze kukimbilia milimani.” (Mt. 24:15, 16) Lakini wafuasi wa Yesu wangetambuaje wakati ambao unabii huo ungetimia?
14. Ni mambo gani yaliyotukia ambayo yalifanya maana ya maagizo ya Yesu yawe wazi zaidi?
14 Matukio yalipoanza, maana ya maneno ya Yesu yalianza kuwa wazi. Katika mwaka wa 66 W.K., majeshi ya Roma yakiongozwa na Sesho Galo yalifika Yerusalemu ili kuzima uasi wa Wayahudi. Wakati waasi Wayahudi, walioitwa Wazeloti, walipokimbilia ndani ya ngome ya hekalu, wanajeshi wa Roma walianza kubomoa ukuta wa hekalu. Wakristo waliokuwa macho walielewa kikamili maana ya mambo yote hayo: Jeshi la kipagani lililobeba sanamu zake (“lile chukizo”) liliukaribia ukuta wa hekalu (“mahali patakatifu”). Huo ulikuwa wakati kwa wafuasi wa Yesu ‘kuanza kukimbilia milimani.’ Lakini wangeondokaje katika jiji ambalo lilikuwa limezingirwa? Mambo fulani yasiyotazamiwa yalikuwa karibu kutukia.
15, 16. (a) Ni maagizo gani hususa ambayo Yesu alitoa, na kwa nini ilikuwa muhimu kwa wafuasi wake kuyatii? (b) Ukombozi wetu utategemea nini?
15 Inashangaza kwamba bila sababu yoyote ile, Sesho Galo na vikosi vyake waliondoka Yerusalemu na kuanza kurudi Roma. Wazeloti waliwafuata na kuwakimbiza. Sasa kwa kuwa Waroma na Wayahudi waasi walikuwa wametoka jijini, kwa ghafula wafuasi wa Yesu walikuwa na fursa ya kukimbia. Yesu alikuwa amewaagiza waziwazi wafuasi wake kutoka bila kukawia na kuacha vitu vyao vya kimwili. (Soma Mathayo 24:17, 18.) Je, kwa kweli ilikuwa lazima kutenda kwa haraka hivyo? Punde si punde, jibu lilikuwa wazi. Baada ya siku kadhaa, Wazeloti walirudi na kuanza kuwalazimisha wakaaji wa Yerusalemu na Yudea wajiunge nao katika uasi. Hali iliharibika haraka jijini wakati vikundi vya Wayahudi wenye kupingana vilianza kupambana ili kudhibiti jiji. Haikuwa rahisi kukimbia. Waroma waliporudi mwaka wa 70 W.K., haikuwezekana kukimbia kutoka Yerusalemu. (Luka 19:43) Mtu yeyote ambaye alisita-sita kutoka jijini alinaswa! Kuhusu Wakristo waliokimbilia milimani, kutii maagizo ya Yesu kuliokoa maisha yao. Walijionea wenyewe kwamba Yehova anajua jinsi ya kuwakomboa watu wake. Ni somo gani tunaloweza kujifunza kutokana na simulizi hilo?
16 Matukio yatakapoanza wakati wa dhiki kuu, Wakristo watahitaji kutii maagizo kutoka katika Neno la Mungu na tengenezo. Kwa mfano, amri ya Yesu ya ‘kuanza kukimbilia milimani’ ina maana katika siku zetu. Hadi sasa haijulikani jinsi hasa tutakavyokimbia.b Hata hivyo, tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atafunua wazi maana ya maagizo hayo wakati utakapofika ili tuweze kuyafuata. Kwa kuwa ukombozi wetu utategemea utii wetu, ni vizuri tujiulize: ‘Je, ninatii maagizo ambayo Yehova anatoa kwa watu wake sasa? Je, ninatii mara moja au ninasita-sita?’—Yak. 3:17.
-
-
Yehova Anajua Jinsi ya Kuwakomboa Watu WakeMnara wa Mlinzi—2012 | Aprili 15
-
-
16 Matukio yatakapoanza wakati wa dhiki kuu, Wakristo watahitaji kutii maagizo kutoka katika Neno la Mungu na tengenezo. Kwa mfano, amri ya Yesu ya ‘kuanza kukimbilia milimani’ ina maana katika siku zetu. Hadi sasa haijulikani jinsi hasa tutakavyokimbia.b Hata hivyo, tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atafunua wazi maana ya maagizo hayo wakati utakapofika ili tuweze kuyafuata.
-