-
Kusaidia Familia Zipate Wakati Ujao Wenye KudumuHuduma ya Ufalme—1997 | Machi
-
-
3 Unaweza kufuatia mazungumzo yako ya kwanza kuhusu maisha yenye furaha ya familia kwa kusema:
◼ “Ningependa kukuonyesha jambo fulani katika kitabu ulichopata ambalo nafikiri utalithamini. Sura ya mwisho yakazia siri yenyewe ya furaha ya familia. [Soma fungu la 2 kwenye ukurasa wa 183.] Angalia kwamba kujitahidi pamoja kufanya mapenzi ya Mungu ndio ufunguo. Twapendekeza kwamba familia zijifunze Biblia pamoja zijue mapenzi ya Mungu ni nini na jinsi ya kuyatumia katika nyumba yao. Twatoa mtaala wa funzo la Biblia bila malipo ambao huchukua miezi michache tu kuumaliza. Ukiniruhusu, nitakuonyesha jinsi linavyoongozwa.” Rudi ukiwa na broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? au kitabu Ujuzi, chochote kitakachofaa zaidi.
-
-
Kusaidia Familia Zipate Wakati Ujao Wenye KudumuHuduma ya Ufalme—1997 | Machi
-
-
5 Unaweza kujenga mazungumzo yako ya kwanza pamoja na kijana kuhusu mawasiliano kati ya mzazi na mtoto kwa kusema:
◼ “Nilithamini kupendezwa ulikoonyesha katika umaana wa kuwa na mawasiliano mazuri katika familia yenu. Je, ungesema ni nini iliyo habari ya maana zaidi ambayo wazazi na watoto wanapaswa kuzungumza?” Ruhusu itikio. Kisha fungua ukurasa wa 68 katika kitabu Furaha ya Familia, na usome jibu linalopatikana katika nusu ya kwanza ya fungu la 11. “Kuwa na funzo la Biblia la kila juma ni njia bora kabisa ya kujipatia ujuzi juu ya Mungu.” Toa broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? Eleza kwamba masomo yayo 16 huandaa muhtasari wa msingi wa ujumbe wa Biblia. Soma utangulizi kwenye ukurasa wa 2, kisha zungumzeni pamoja somo la kwanza.
-
-
Kusaidia Familia Zipate Wakati Ujao Wenye KudumuHuduma ya Ufalme—1997 | Machi
-
-
7 Katika ziara yako ya pili kwa mzazi aliyekubali kitabu “Furaha ya Familia,” unaweza kuendeleza mazungumzo kwa njia hii:
◼ “Tulipokutana mara ya kwanza, niliweza kuona kwamba unajali kikweli kuhusu watoto wako na kwamba unataka kufanya yote uwezayo kuwalinda na mavutano mabaya. Huenda bado hujasoma kile kitabu nilichokuachia, lakini kuna maoni ya maana ndani yacho unayopaswa kuona. [Soma fungu la 19 kwenye ukurasa wa 59.] Kusitawisha uhusiano pamoja na Mungu kwahitaji kumjua kupitia Neno lake lililoandikwa, Biblia. Je, ungependa nikuonyeshe jinsi tunavyojifunza Biblia tukiwa familia?”
-