Kiliwasaidia Waache Kupigana
Mvulana mmoja mwenye umri wa miaka 11 wa California, Marekani, aliandikia Mashahidi wa Yehova katika Brooklyn, New York:
“Navipenda vitabu vyenu, hasa Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Kabla hatujapata kitabu hicho, dada yangu nami hatungeacha kupigana kamwe. Siku moja tuliamua kujifunza kitabu hicho, na tukatambua ya kwamba hatukuwa tukifanya vile Mungu alivyotaka tufanye.
“Kitabu hiki kilitusaidia sana. Ninakithamini sana, na ninatia moyo familia nyingine zikisome kwa sababu ni kizuri sana. Pia kinaisaidia familia yetu kupata amani na furaha nyumbani.”
Siri ya Kupata Furaha ya Familia ni kitabu chenye kurasa 192 ambacho hushughulikia habari yenye msaada kama vile “Ilinde Familia Yako Dhidi ya Mavutano Yaletayo Uharibifu,” “Dumisha Amani Nyumbani Mwako,” “Unaweza Kushinda Matatizo Yanayoidhuru Familia.”
Ikiwa ungependa mtu aongoze funzo la Biblia nyumbani bila malipo pamoja nawe, andikia I.B.S.A. Box 47788, Nairobi, Kenya, au kwa anwani ihusuyo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5.